Na Shomari Binda
Musoma,
JUMLA
ya Watoto 30 wanaoishi na Ulemavu Mkoani Mara wanatarajiwa kujiunga na
Elimu ya Sekondari pamoja na mafunzo mbalimbali ya ufundi yakiwemo ya
computer yanayowezeshwa na kituo cha kuhudumia watu wanaoishi na Ulemavu
cha CBR-Mara kilicho chini ya Kanisa la Anglican Jimbo la Musoma.
Akinzungumza na Blog hii
Ofisini kwake Mratibu wa CBR Dokta Hennry Yoggo alisema moja ya mipango
ya kazi ya CBR kwa mwaka 2013 ni pamoja na kuwawezesha watoto wenye
Ulemavu ambao wapo katika familia zisijojiweza kuhakikisha wanapata
elimu ikiwemo ya ufundi ili kuja
kujitegemea katika maisha ya baadae na kuepukana na utegemezi.
Alisema
katika ofisi yake tayari wameshapokea maombi 30 ya watoto wenye ulemavu
wakiwemo wa elimu ya sekondari pamoja na mafunzo mbalimbali ya ufundi
ambao tayari
wameshawafanyia utaratibu wa kuwalipia karo tayari kwa kujiunga na
muhula wa masomo wa mwaka 2013.
Yoggo alisema
Jamii inapaswa kuwajali watoto wanaoishi na Ulemavu katika kuwaandalia
mazingira mazuri kikubwa ikiwa ni elimu ambayo itawawezesha kupata ujuzi
ambao utawasaidia katika maisha na kuepukana na utegemezi kwa sababu tu
wamezaliwa wakiwa na ulemavu.
" CBR-Mara katika kipindi cha mwaka 2013 tunazo
program mbalimbali ikiwemo ya kuwasomesha watoto wanaoishi na ulemavu
ikiwa na lengo la kuwatengenezea mazingira ya kielimu ambayo
yatawasaidia kujishughulisha baada ya kuipata na kuepukana na masuala ya
uegemezi na kujiona wa hali ya chini wakati wote.
"Watoto wanaoishi na ulemavu hawapaswi
kutengwa kutokana na ulemavu walio nao bali ni wajibu wa jamii
kushirikiana na kuona namna gani ambayo inapaswa kuchukuliwa ili
kuwawezesha kupata elimu ambayo itakuwa msingi mkubwa katika maisha yao
ya baadae,"alisema docta Yoggo.
Aidha
Mratibu huyo wa CBR-Mara alidai licha ya kuwa na programu hiyo ya
kusomesha watoto wanaoishi na ulemavu pia katika kipindi cha mwaka 2013
watakuwa na mpango wa kutoa elimu kwa Wanawake ya uzazi salama ili
kujiepusha na ulemavu unaotokana na uzazi.
Alisema
katika tafiti zilizofanywa imeonekana baadhi ya kina mama waamekuwa
hawazingati mahudhulio ya kliniki hali inayosababisha kutokupata elimu
juu ya uzazi salama na kupelekea kuleta matatizo katika kujifungua na
kupelekea ulemavu wakati wa uzazi.
"Hii pia itakuwa ni program kubwa ya utoaji elimu kwa Wanawake juu ya uzazi salama na tumejipanua zaidi katika hili maana tutafika katika wilaya za Bunda,Butiama pamoja na musoma lakini kwa baadae tutafika katika maeneo yote ya mkoa wa Mara.
"Lakini elimu pia tutaitoa
kwa wahudumu wa Afya pamoja na wakunga lengo likiwa kuhakikisha
Mwanamke anapata elimu ya kutosha juu ya uzazi salama ili kuepukana na
ulemavu ambao unaweza kutokea wakati wa kujifungua,"aliongeza.
Alidai
baadhi ya Wanawake wamekuwa hawazingatii tiba za awali na mahudhurio ya
kliniki wakati wa ujauzito na kupelekea kuzaliwa watoto wenye ulemavu.
Home
»
»Unlabelled
» WATOTO 30 WANAOISHI NA ULEMAVU KUSOMESHWA NA CBR-MARA
Post a Comment
0 comments