MKUU WA WILAYA YA BUTIAMA AKIWA KATIKA PICHA NA WANAFUNZI WA KIKE WA SHULE MBALIMBALI WILAYANI HUMO BAADA YA KONGAMANO
WANAFUNZI wa kike 2,425 katika shule
mbalimbali za Sekondari wilaya ya Butiama mkoani Mara,
wameshindwa kuendelea na masomo yao ya Sekondari kutokana
na sababu mbalimbali ikiwemo ya kupata
mimba na kulazimishwa kuolewa na wazazi wao.
Mkuu wa wilaya ya Butiama Angelina Mabula,ametoa taarifa
hiyo katika kongamano la kujadili hali ya
elimu kwa watoto wa kike wilayani humo, huku akisema wanafunzi hao
ni kati ya 7,818 walijiunga na kidato cha kwanza katika
kipindi cha miaka mitatu.
Amesema idadi hiyo ni kubwa na inarudisha nyuma maendeleo ya elimu
kwa mtoto wa kike hivyo serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu
lazima kuhakikisha inapambana na hali hiyo.
Mabula ameeleza kuwa suala la elimu haliwezi kuachwa nakuona
wanafunzi wa kike wakipata mimba na kuozwa na wazazi na kutaka kila mmoja kutoa
taarifa anapoona jambo hilo hili yoyote anayehusika na kukwamisha maendeleo ya
elimu aweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Mkuu huyo wa Wilaya amesema katika siku za hivi
karibuni imebainika tena kuna wanafunzi wengine
wa kike zaidi ya 40 wamegundulika kuwa na ujauzito katika
halmashauri ya Butiama wakati uchunguzi ukiendelea katika halmashauri ya
Musoma.
Kwa upande wake mgeni rasmi katika kongamano hilo,Katibu Mkuu Umoja
wa Wanawake Tanzania (UWT) Amina Makilagi,pamoja na kusikitishwa na
ukubwa wa tatizo la vikwazo vya elimu kwa
mtoto wa kike wilayani Butiama,amewataka wanafunzi hao
wa kike kutoka shule mbalimbali za sekondari
wilayani humo,kuepukana na vishawishi ambavyo alisema
vinaweza kukatisha ndoto zao katika maisha.
Amesema lazima mtoto wa kike asome aweze kukabiliana na
changamoto mbalibali za maisha na kila mmoja asikubali kuona motto wa kike
akiishia kupata mimba na kuozwa akiwa anasoma.
Makilagi amewataka watoto wa kike kujitambua na kulipa kipaumbele
suala la elimu kama nguzo kuu ya maisha na pale wanapoona mtu yoyote anataka
kumuharibia msingi wa maisha kumtolea taarifa kwenye vyombo vya dola.
Post a Comment
0 comments