Akihutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kusikiliza mkutano huo,mgombea udiwani wa Kata hiyo,Charles Mwita,amesema kutokana na heshima waliomuonyesha wananchi kwa kujitokeza kwa wingi,atahakikisha anawalipa maendeleo pale atakapofanikiwa kushinda kwenye uchaguzi oktoba 25.
Mwita amesema imani waliomuonyesha kwenye mkutano huo waendelee kumuonyesha hadi ifikapo oktoba 25 kwa kumpigia kura za kishindo pamoja na mgombea urais John Pombe Magufuli na mgombea wa nafasi ya ubunge wa Jimbo la Musoma mjini,Vedastus Mathayo.
Akizungumza kwenye mkutano huo,Katibu wa CCM wilaya ya Musoma mjini,Jacob Nkomola,amesema wananchi wamechoka kudanganywa na sasa wameamua kukiamini chama hicho na hilo limekuwa likijihidhilisha kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mikutano.
Amesema mkutano wa kesho utakaofanyika Kata ya kwangwa,utahudhuliwa na mgombea ubunge wa Jimbo la Musoma mjini na kuwaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kusikiliza sera za chama hicho na kufanya maamuzi sahihi oktoba 25.
MRS.MWITA AKIOMBA KURA ZA MZEE
MWITA AKIOMBA KURA KWA WANANCHI
Post a Comment
0 comments