Ushauri huo ulitolewa na Mganga Mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara,Elias Godfrey,wakati akishiriki zoezi la kupima afya za wachezaji wa klabu ya Biashara United,lililofanyika kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Karume mjini hapa.
Elias alisema kila mchezaji anapaswa kuzingatia suala la kuangalia afya yake na sio vizuri kushiriki michezo kwa muda mrefu bila kutenga muda wa kufanya vipimo na kujua maendeleo ya afya.
"Tumewahi kuwashuhudia baadhi ya wachezaji wakipata matatizo na wengine wakipoteza maisha wakiwa mchezoni hivyo ni muhimu kuwa na utaratibu wa kupima afya kwa kila mchezaji na ni vyema viongozi wa klabu nyingine wakawa na utamaduni huu",alisema Elias.
Mwenyekiti wa klabu ya Biashara United,Selemani Mataso,alisema kwa kujua umuhimu wa kuangalia afya kwa wachezaji,waliamua kujipanga na kufanya zoezi hilo huku akidi litakuwa endelevu kwenye klabu hiyo na kutoa wito kwa klabu nyingine kuwa na utaratibu wa kuangalia afya za wachezaji.
LUZUNDANA AKIPATA USHAURI WA DOCTA BAADA YA VIPIMO
GEORGE AKIFATILIA MAELEZO YA DOCTA
KATOGORO HAKUWA NYUMA KUANGALIA AFYA
SHOMMI B BLOG PIA NI MMOJA WAO
SHUKU MMOJA WA MCHEZAJI KIONGOZI WA TIMU YA BIASHARA
FOLENI KWAAJILI YA VIPIMO
Post a Comment
0 comments