Mpango huo umeanza kwa kufundishwa waamuzi wa soka ngazi ya awali kama alivyotoa ahadi Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Mara,Michael Wambura,mara baada ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo miezi michache iliyopita.
Amesema mpango huo utaweza kuzalisha waamuzi wengi kwenye wilaya mbalimbali za mkoa kwa kuwa waamuzi hao wametoka kwenye maeneo ya wilayani ambapo kumekuwa na uhaba mkubwa wa waamuzi.
Sangawe amesema kutokana na kukosekana kwa waamuzi wa kutosha kulipelekea kuibua migogoro ambayo inahusiana na maamuzi na kuwaomba wanaosomea fani hiyo kuzingatia mafunzo yote watakayofundishwa.
Amesema sheria namba 12 ya mchezo imebadilika ambapo kosa linaweza kuchezwa nje ya uwanja na kisha adhabu ikaja kuchezwa uwanjani hivyo kila mmoja wakiwemo waamuzi na makocha ni muhimu kufahamu na kushukuru (FAM) kwa kuandaa mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo walitoa pongezi upatikana kwa mafunzo hayo na kudai kutokana na kuupenda mchezo huo wamekuwa wakichezesha michezo mbalimbali bila kuzijua sheria na kudai baada ya mafunzo hayo na menine watakayoyapata kutawafanya kuwa waamuzi bora.
Elimu ikiendelea darasani
Baadhi ya waamuzi watarajiwa wakizungumzia elimu wanyoipata
Post a Comment
0 comments