0


CCM Mara yawakataa Wabunge A.Mashariki
     
-Nyerere amfuata Bhanj kuanguka
    -Akubali matokeo na kukataa makundi
    -Adai kama yataendelea CCM isitegemee ushindi

Na Shomari Binda
      Musoma,

Ni kama ambavyo unaweza kusema Chama  cha Mapinduzi Mkoani Mara haina haja na haiwataki Wabunge wa Afrika Mashariki baada ya kuwaangusha katika chaguzi zinazoendelea ndani ya Chama hicho Nchi nzima katika nafasi mbalimbali za uongozi.

Katika uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi Mkoani mara wajumbe wa mkutano huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wajumbe walimpigia kura ambazo hazikutosha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho katika miaka mitano iliyopita Charles Makongoro Nyerere ambaye pia ni Mbunge wa Afrika Mashariki na kumchagua Christopher Sanya ambaye kisiasa ni mlezi wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Bunda.

Katika uchaguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Shule ya Wasichana ya Songe High School licha ya kuwashirikisha wagombea watatu katika nafasi ya Mwenyekiti ushindani tangu mwanzo ulikuwa kwa 
 Makongoro Nyerere na Christopher Sanya hali iliyopelekea kurudiwa kwa duru ya pili kwa wagombea hao huku mgombea mwingine Mwenyekiti wa zamani wa Chama hicho Mkoani Mara Mwita Chambiri akishindwa vibaya katika duru ya kwanza.


Blog hii iliwashuhudia wapambe na wapiga debe wa kila mgombea wakihaha nje ya ukumbi wa mkutano huo kutafuta kura kwa wajumbe huku kila upande ukionekana kumbana mwenzake asitumie matumizi ya fedha katika kuwarubuni wajumbe huku baadhi ya wajumbe wakipasha kuwa hawa wanaangaika si tulishakula chetu kuanzia jana (juzi).

“Sisi tumeshukula chetu tunachosubili ni muda wa kupiga kura ufike tumalize kazi tumeshapewa maelekezo na hapa lazima tushinde maana kiasi tulichopewa si haba na lazima tutashinda tumechoka,”alisikika mmoja wa wajumbe akizungumza lakini hakuonyesha yupo kwa mgombea gani.

“Takukuru inabidi watafute njia nyingine mbadala ya kudhibiti Rushwa naomba nikuhakikishie ngugu yangu lakini usitaje jina langu, uchaguzi huu matumizi makubwa ya fedha yametumika na kuhakikishia hivyo nikiwa kama mjumbe na tukiendelea hivi sijui kama tutafika kwa kumpata kiongozi chaguo sahihi”,aliongea mmoja wa wajumbe aliyedai anatoka katika Wilaya ya Butiama.

Licha ya kuwepo na harakati za kutafuta kura kwa wapambe kwa kupita huku na kule hali ya usalama ilihimalishwa katika uchaguzi huo kwa kuwadhiti wale wasiokuwa wajumbe kuingia katika ukumbi wa mkutano wa uchaguzi huku vitambulisho maalum vikitengenezwa kwa wale waliotakiwa kushuhudia uchaguzi huo
Msimamizi wa uchaguzi huo Nazir Karamagi (MB) alimtangaza Christopher Sanya majira ya saa sita usiku kuwa Mwenyekiti wa chama cha Mapaindizi Mkoani Mara kwa kupata kura 481 na kumzidi Makongoro Nyerere aliyepata kura 422 katika duru ya pili ya uchaguzi huo.

Katika matokeo ya awali yaliowahusisha wagomea watatu Mwita Chambiri alipata kura 140,Charles Makongoro Nyerere alipata kura 371 huku Christopher Sanya akipata kura 500 lakini hazikumuwezesha kushinda kutokana na kutofikia asilimia 50.

Katika maneno yake ya shukrani Charles Makongoro Nyerere alikubaliana na uwamuzi wa wajumbe kutokana na kura alizopata na kushindwa kutosha na kutoa tahadhari ya kuepukana na makundi ambayo kama yataendelea kuwepo katika Chama hicho katika chaguzi zinazo kuja kitapoteza Mitaa,Vijiji,Vitongoji na Majimbo mengi.  

“Mimi nimepitia katika kipindi kigumu sana cha miaka yangu mitano ya uongozi sikutaka kupinda na nilikuwa imara na huenda ndio kimenigharimu na leo,lakini hayo yamepita na namtaka mrithi wangu awe imara na asikubali kuyumbishwa  la sivyo miaka 5 ataiona michungu kiuongozi.

“2014 na 2015 kuna uchaguzi wa Serikali za mitaa pamoja na uchaguzi mkuu wa Mwaka 2015 bila kuwaunganisha hawa wajumbe kuwa wamoja na kukusaidia katika masuala mbalimbali hakuna ushindi ambao utaweza kupatikana  katika chaguzi hizo,”alisema Makongoro.

Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Mara Christopher Sanya alihaidi kuufanyia kazi ushauri uliotolewa na mtangulizi wake ili yale yaliyomsukuma kuomba nafasi hiyo na kuaminiwa kupewa yaweze kutekelezeka.

Sanya alisema atajitahidi kadri ya uwezo wake kuweza kutokubaliana na kuyapa nafasi makundi katika kipindi chake cha uongozi na kumpa nafasi kila Mwanachama kutoa maoni na ushauri wake katika kufanikisha kile ambacho kinatarajiwa.
Charles Makongoro Nyerere anaungana na Mbunge mwenzake wa Bunge la Afrika Mashariki Shy –Rozi Bhanj kukataliwa na wanachama wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Mara baada ya Bhanj kuangushwa na Agnes Marwa katika nafasi Mjumbe wa Baraza la Taifa (UWT) katika uchaguzi wa Jumuiya hiyo Mkoani Mara.




Post a Comment