BAADHI YA WACHEZAJI WA TIMU YA POLISI MARA WAKIWAFATILIA WENZAO WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI |
Kikosi cha timu ya
maafande wa Polisi Mara wamepania kuibuka na ushindi katika mchezo wao wa
kwanza wa ligi daraja la kwanza Tanzania Bara dhidi ya Pamba ya Mwanza TP
lindanda utakaopigwa kwenye dimba la CCM Kirumba oktoba 24 ikiwa ni safari ya
kuelekea katika ligi kuu ya Vodaco katika msimu ujao.
Akizungumza na Blog hii katika mazoezi ya timu hiyo kwenye
uwanja wa kumbukumbu ya Karume Mjini Musoma,Mwenyekiti wa timu hiyo Inspekta
Alon Mihayo amesema kutokana na mazoezi ambayo timu yake imeyafanya chini ya
kocha mkuu wa timu hiyo Hafidh Salim akishirikiana na benchi la ufundi
wanaamini watafanya vizuri na kupanda ligi kuu.
Amesema program zote ambazo kocha amekuwa akizihitaji
zimefanyika kama ilivyotakiwa hivyo kilichobaki ni kusubili siku ifike ili
waone kile walichopanda ila anaamini kwa hali waliyonayo wachezaji watafanya
vizuri na kufikia malengo waliyopanga.
Mihayo amesema wamekuwa wapo karibu na wachezazi wote
waliowasajili na kila mmoja kutekelezewa mahitaji yake na kudai kuwa watafanya
kile ambacho wanatakiwa kukifanya ikiwa ni kuhakikisha wanashilikiana na
uongozi ili kuweza kufanya vizuri kwenye ligi.
Mwenyekiti huyo wa kikosi cha maafande wa Polisi Mara
ameongeza kuwa wanahitaji pia sapoti ya nashabiki na wadau wa timu hiyo katika
mchezo wa ufunguzi jumatano ya octoba 24 katika dimba la kirumba hivyo yeyote
atakaye weza kujisafirisha afanye hivyo ili kuweza kwenda kuitia nguvu timu
katika mchezo huo muhimu.
Amesema iwapo watashinda katika mchezo huo utawaongezea hali
ya kufanya vizuri katika mchezo wao wa pili octoba 27 dhidi ya Mwadui ya
Shinyanga utakaofanyika katika uwanja wa Kambarage Mkoani humo
Post a Comment
0 comments