MTU
mmoja aliyemtapeli Mkuu wa mkoa wa Mara na Maafisa wa Usalama mkoani
hapa amehukumiwa kwenda jela
miaka mitatu baada ya kujitambulisha kuwa yeye ni Afisa Usalama kutoka
Makao Makuu anahitaji Ulinzi wa Usalama dhidi yake ili kufikia adhima
yake ya kutambua uuzaji wa risasi na bunduki kutoka Kikosi cha Jeshi cha
27KJ mkoani hapa.
Awali
akisoma hukumu hiyo hakimu mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Musoma Richard
Maganga alisema ushahidi uliotolewa mahakamani hapo ulidai Juni 17
mwaka huu mtuhumiwa aliyemtaja kwa jina la Liso Chacha alimpigia simu Mkuu wa mkoa
John Tupa kuwa yeye ni Afisa Usalama toka Makao Makuu aliyeagizwa kuja mkoani Mara
kwa lengo la kufuatilia mtandao wa kuuza risasi na bunduki kutoka katika kikosi
cha jeshi 27 KJ kilichopo Makoko.
Hakimu
Maganga
alisema baada ya RC kupata taarifa hizo alimpigia simu Mkuu wa Kikosi
cha Jeshi cha Makoko akimtaka kuwasiliana na mtuhumiwa huyo kwa lengo la
kufanikisha shughuli iliyomleta Afisa huyo tapeli.
Maganga
alisema
katika ushahidi uliotolewa mahakamani hapo wa watu saba wa upande wa
mashitaka ulikuwa
ukimtuhumu mshitakiwa kuwa alikuwa akijitambulisha kuwa yeye ni Afisa wa
Usalama kutoka Makoa Makuu na kuwataka wampe ushirikiano katika
kufuatili
mtandao wa wizi wa risasi na bunduki uliokithiri mkoani Mara.
Alisema mshitakiwa huyo alipokelewa na Afisa wa Jeshi na kumpa malazi katika nyumba ya
mapumziko ya jeshi na kumgharamikia chakula na huduma zingine muhimu ikidhaniwa ni Ofisa wa Usalama wa Taifa kama alivyojieleza.
Hakimu
Maganga
aliendelea kusema siku iliyofuata Afisa huyo wa Jeshi alimfuata Afisa
wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Kutuliza Ghasi(FFU) kwa lengo la kumsaidia
kumpa
ulizi wa kumsindikiza mtuhumiwa huyo kufanya upekuzi kwa baadhi ya
magari
aliyowatajia kuwa yatapita katika beria ya polisi iliyopo eneo la
Kirumi.
Afisa
huyo pia alimpatia askari wawili ambao waliambatana nao katika eneo hilo na
kuanza kukagua magari kwa muda wa siku mbili bila kufanikisha kitu
chochote,hivyo wakawa wamejipanga kurudi tena kwa siku ya tatu.
Hakimu
alisema kabla hawajaondoka siku hiyo ya tatu mtuhumiwa huyo aliingia katika Ofisi ya
wanahabari kwa lengo la kutaka msaada kutoka kwao lakini
mahojiano na wanahabari hao walimshutukia na kutoa taarifa kwa Afisa Usalama wa
mkoa na maeneo mengine hali iliyopelekea kumtia hatiani kwa wakati ule.
Kwa upande
wa Idara ya Usalama wa Taifa Makao Makuu walipoulizwa kuhusiana na tuhuma za mtuhumiwa
huyo walidai hawajamtuma mtu kufanya shughuli ya aina hiyo mkoani hapa na
kwamba katika orodha ya watumishi wa Usalama wa Taifa hapa nchini hakuna jina
kama hilo,ilieleza sehemu ya Hukumu hiyo.
Hakimu
alisema ni kinyume cha Sheria na taratibu mtu kujitambulisha kwa
nafasi isiyo yake na kwamba mshitakiwa anahitaji adhabu kali na adhabu kubwa
kulingana na kosa hilo alilofanya ni kutumikia jela miaka mitano,lakini
kufuatia maombi ya mtuhumiwa kuwa anao watoto wanaomtegemea atatumikia kifungo cha miaka mitatu jela.
Mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi Stephano Mgaya aliiambia Mahakama
kuwa mtuhumiwa alifanya kosa la jinai kuidanganya Serikali na kuchafua vyombo vya dola kuwa ni mtumishi wa
umma na pia ameagizwa na idara ya Usalama Makao Makuu kufanya uchunguzi wa
mtandao wa wizi wa silaa jambo ambalo ni uongo.
Mgaya
alisema mtuhumiwa anastahili adhabu kali kwa kuipaka Serikali matope ili
iwe fundisho kwake na kwa watu wengine wenye tabia ya kufanya udanganyifu wa kujipa nyadhifa ambazo sio zao na kufanya utapeli.
Baada
ya Hukumu ya kufungwa miaka mitatu mtuhumiwa huyo,baadhi ya wananchi
waliokuwa nje ya Mahakama kwa lengo la kusikiliza hukumu
hiyo walidai uongozi wa Usalama mkoani hapa hauna maana kama mtu wa
kawaida ananweza kuwaeleza jambo na wakamfuata bila hata kumuhoji ni
hatari kubwa.
"Haiwezekani kwa muda wa siku tatu maafisa wa Usalama wa JWTZ NA Polisi kushindwa kumtambua mtu huyo na kumpa hifadhi zote katika makazi ya maafisa wa jeshi hadi Waandishi wa Habari wamshuku ndio hakamatwe hii ni hatari kubwa ya kiusalama.
"Haiwezekani kwa muda wa siku tatu maafisa wa Usalama wa JWTZ NA Polisi kushindwa kumtambua mtu huyo na kumpa hifadhi zote katika makazi ya maafisa wa jeshi hadi Waandishi wa Habari wamshuku ndio hakamatwe hii ni hatari kubwa ya kiusalama.
“Ningekuwa
mimi ndio Hakimu huyu jamaa ningemfunga siku moja tu,manake wenye kutambua kuwa huyu ni
mdanganyifu ni viongozi wa usalama wa mkoani hapa,kwa kuanzia kwa mkuu wa mkoa”alisema
Daniel Nyasaungu.
Post a Comment
0 comments