0





KATIKA kuendeleza michezo Manispaa ya Musoma,Mjumbe wa Halimashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi(CCM)wilayani Musoma,Vedastus Mathayo,ameialika timu ya vijana ya Azam FC kucheza michezo miwili ya kirafiki na kombani ya vijana wa Musoma.

Akizungumzia kuhusiana na kualikwa kwa timu hiyo,mratibu wa mashindano ya kukuza vipaji ya Mathayo Cup yanayofanyika kila mwaka mjini Musoma,Amani Richard,amesema muandaaji wa mashindano hayo amekusudia kuleta mabadiliko ya soka Manispaa ya Musoma na mkoa wa Mara kwa ujumla na kuahidi kuzialika timu mbalimbali kwaajili ya changamoto za michezo.
 
Amesema Mathayo amekubali kugharamikia malazi na chakula na huduma nyingine kwa timu ya vijana ya Azam kwa siku 2 itakazokuwa Musoma na tayari wamekwesha watumia barua uongozi wa timu hiyo na wanachokisubilia ni majibu kutoka kwa timu hiyo.

Amani amesema timu ya kombaini ya Musoma imepatikanakutoka kwenye mashindano ya mwaka huu yanayofikia tamati desemba 10 kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Karume mjini hapa ambapo jumla ya timu kutoka Kata 13 za Manispaa ya Musoma zimeshiriki na kupatikana vipaji vingi vya vijana.



“Tunashukuru kwa fursa hii nzuri ambayo tumeipata kutoka kwa muaandaaji wa mashindano ya Mathayo Cup kwa kuialika timu ya vijana ya Azam FC kwa kuwa ni fursa nzuri kwa vijana wa Musoma kuweza kuonyesha vipaji vyao.

“Tayari tumeshatuma barua kwa uongozi wa timu ya Azam FC na tunaamini kwa kuwa ni watu wa michrzo na wanaofanya jitihada katika kuendelea soka hususani soka la vijana watatukubalia ombi letu na kuhakikisha timu yao inafika Musoma na kucheza michezo hiyo ya kirafiki,alisema Amani”.

Amesema katika barua yao wameiomba timu hiyo kucheza michezo 2 kwenye uwanja wa Karume kati ya desemba 13 na 14 na tayari wakazi wa Manispaa wameshakuwa na hamu ya kuiona timu ya vijana ya Azam ikicheza na kombaini ya Musoma.

Akizungumzia mualiko huo kwa njia ya simu,Meneja wa timu ya Vijana ya Azam FC  Philipo Alando amesema wamepokea barua kutoka kwa mratibu wa mashindano ya Mathayo Cup yanayofanyika Musoma kwa lengo la kucheza michezo hiyo ya kirafiki na jibu kamili na jibu kamili linatarajiwa kutolewa wakati wowote na uongozi wa Azam.




Post a Comment