0

WACHUNGAJI wa madhebu ya Dini katika wilaya ya Musoma mjini,wamewakemea viongozi wa vyama vya siasa wanaopanda kwenye majukwaa na kugomesha michango ya maendeleo.

Wakizungumza katika mkutano wa wadau wa elimu uliohitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Musoma,Jackson Msome,katika ukumbi wa uwekezaji wa mkoa wa Mara,viongozi hao walisema sio jambo la busara kuwahamasisha wananchi kuacha kuchangia maendeleo yao hususani sekta ya elimu.

Waliema kwenye maeneo mengine ya nchi,wananchi wamekuwa mstari wambele kuchangia maendeleo yao na kupata mafanikio lakini kwa Musoma hali imekuwa tofauti huku viongozi wa kisiasa wakiwa mbele kuwagomesha wananchi wasichangie.

Mchungaji wa Kanisa la Evangelistic Asemblius of God(EAGT) Moses Sephania, alisema siasa isiweze kuwafanya watu kuacha masuala ya msingi na kuahamasika kuacha kuchangia ujenzi wa maabara mashuleni jambo ambalo litapelekea kuzalisha wanafunzi wasioweza kuendelea na masomo ya juu.

Alisema suala la maabara ni jambo la msingi katika maendeleo ya elimu na kama kuna mwanasisa anayepanda kwenye majukwaa na kutoa maneno ya kugomesha kuchangia atoe sababu za msingi za kutokufanya hivyo.

 Kwa upande wake,Askofu wa Kanisa la New Life Church,Daniel Ouma Dawa,alisema anachoweza kukifanya na kuwakemea kwa nguvu za Mungu wale wote wanaogomesha michango ya maendeleo kwa kuwa sio watu wema katika Wilaya ya Musoma.

“Kwa jina la Yesu,watu hawa washindwe na kuwaacha wananchi huru ili waweze kuchangia maendeleo yao ya elimu na kuweza kujikomboa katika soko la ajira,sisi hatutachoka kuhamasisha katika nyumba za ibada ili kutambua umuhimu wa kuchangia elimu,”alisema Askofu Dawa.

Awali akifungua mkutano huo uliowashirikisha watu wa kada mbalimbali na wadau wa elimu,Mkuu wa Wilaya ya Musoma,Jackson Msome,alisema wanaendelea kutekeleza agizo la Rais Kikwete juu ya ujenzi wa maabara lakini kuna wanasiasa wanaowapotosha wananchi na kuwakataza kuchangia.

Alisema kuanzia sasa ametoa agizo katika vyombo vya dola juu ya kuwashughulikia wale wote wanaopotosha suala la ujenzi wa maabara kwa kuwa wanaendelea kuwarudisha nyuma wananchi juu ya kujiletea maendeleo.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema ujenzi wa maabara umefikia asilimia 60 na kuwataka watendaji kuendelea na uhamasishaji wananchui juu ya umuhimu wa kuchangia na kujiepusha na maneno ya wanasiasa wanayoongea majukwaani.







Post a Comment