0
MENEJA MAUZO WA TBL POLYCALIPO MAKUJA AKIWA KATIKA FAINALI ZA MWAKA JANA JIJINI MWANZA

Jumla ya washiriki 80 wakiwemo wanaume hamsini na wanawake ishirini wamejitokeza hadi kufikia siku ya jana tayari kwa kushiriki mashindano ya mitumbwi ya BALIMI Mkoani Mara yatakayofanyika siku ya jumamosi katika fukwe za Bwalo la Maafisa wa Polisi Mwisenge Manispaa ya Musoma.


Akizungumza na Blog hii,Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya TBL Policalipo Makunja  amesema kuwa watu wengi wameendelea kujitokeza kujiandiksha katika Mwalo wa Mwigobero kwa Paschal Matiku na inaonyesha mashindano ya Mwaka huu yatakuwa na ushindani mkubwa kutokana na hamasa iliyopo.


Amesema hamasa nyingine ambayo  imeongezaeka katika Mashindano ya Mwaka huu ni  kuongezwa kwa zawadi ambapo mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume ataondoka na kitita cha shilingi laki tisa,wa pili laki 7,wa tatu laki 5,wa nne laki 4 huku mshindi wa tano hadi wa kumi wataondoka na kila mmoja shilingi laki mbili na nusu.

Kwa upande wa wanawake ataondoka na shilingi laki saba,wa pili laki sita,wa tatu laki tano,wa nne laki 4 huku mshindi wa tano hadi wa kumi kila mmoja kuondoka na shilingi laki mbili.

Poly amesema bado kuna nafasi kwa wale watakaohitaji kushiriki mashindano hayo ambayo fainali zake zitafanyika Jijini Mwanza ambapo wanaweza kujiandikisha kupitia kwa Paschal Matiku ama katika gari la uhamashishaji wa mashindano hayo  lililoanza uhamasishaji tangu siku ya jana na leo jioni watakuwa na uhamasishaji katika Bar ya Keryo garden Mjini Musoma.


Akizungumza sababu za kupeleka mashindano hayo katika Bwalo la Polisi tofauti na mwalo wa Mwigobero ambapo yamekuwa yakifanyika kila Mwaka,Poly amesema ni kupeleka burudani katika maeneo mengine lakini pia uwepo wa kivuko cha katika eneo la Mwigobero pia ni sababu nyingine ya kufanyia mashindano hayo katika fukwe za Bwalo la Polisi.
 




Post a Comment