Na Shomari Binda
Musoma,
Uongozi wa timu ya
maafande wa Polisi Mara inayoshiriki ligi daraja la kwanza imewataka wachezaji
wote wa timu hiyo ambao bado hawajajiunga katika mazoezi ya maandalizi ya
mzunguko wa pili kufanya hivyo ili kuweza kufanya mazoezi ya pamoja.
Akizungumza na
Waandishi wa Habari,Katibu Mkuu wa klabu hiyo Adamu Chiguma alisema baada ya
mapumziko kutokana na kumalizika kwa mzunguko wa kwanza bado kuna wachezaji
ambao hawajawasili katika mazoezi ya timu hiyo tangu yalipoanza majuma matatu
yaliyopita.
Alisema ni muhimu kwa
wachezaji wote kufanya mazoezi ya pamoja ili kuweza kukabiliana na mzunguko wa
pili wakiwa kitu kimoja kutokana na kila timu kupania mzunguko huo ili kuweza
kujiweka katika nafasi nzuri ya kucheza ligi kuu msimu ujao pamoja na kuepuka
kushuka daraja.
Chiguma alisema licha
ya kuweepo na changamoto mbalimbali katika klabu hiyo ikiwemo baadhi ya
wachezaji kudai fedha zao za usajili lakini ni vyema kufika katika mazoezi na
kuweza kuzungumza kwa pamoja ili kuweza kuunda kitu kimoja katika timu.
Alisema amepata
taarifa zisizo rasmi kuwa kuna baadhi ya wachezaji ambao wameshindwa kujiunga
na timu hiyo kwa madai ya kutaka fedha zao za usajili ambazo walihaidiwa kupata
mara baada ya kumalizikakwa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo.
Katibu wa maafande
hao wa Polisi Mara ambao wanashika nafasi ya tano katika msimamo wa kundi c
linaloongozwa na timu ya Rhino ya Tabora alisema kila kitu kinaweza
kuzungumzika na kufikia muafaka hivyo wachezaji ambao bado hawajajiunga kwa
madai ya kutaka feha za usajili huku wakiwa hawaonekani wanakuwa hawatendi
haki.
Katika hatua nyingine
Chiguma amewaomba wadau wa soka katika Mkoa wa Mara kuichulia timu hiyo kuwa ni
timu ya Mkoa mzima wa Mara hivyo kuwa nayo karibu na kuweza kusaidia katika
matatizo mbalimbali ambayo yanaikabili timu hiyo kabla ya kuanza kwa mzunguko
wa pili wa ligi daraja la kwanza ambayo tayari imekwisha tangazwa na TFF kuanza
kutimua vumbi Februari 2.
Alisema kwa kuanzia
timu hiyo inahitaji zaidi ya shilingi milioni 15 ili kujipanga na kuanza mzunguko
wa lala salama wa ligi hiyo ambayo imekuwa na ushindani huku kila timu kwa sasa
ikionekana kuwa katika maandalizi mazito ili kuweza kukabiliana na mikikimikiki
ya ligi hiyo.
Post a Comment
1 comments:
Fani na kasabila nawaaminia apo