Bunda,
WAKULIMA wa
wilaya ya Bunda Mkoani Mara,wameanza kuachana na kilimo cha zao la pamba na
hivyo kuelekeza nguvu zao katika kilimo cha mazao ya Mpunga na Mahindi ikiwa ni
mwaka mmoja tu baada ya kushuka kwa bei
ya zao la Pamba katika soko la dunia hatua ambayo idaiwa kuwasababishia hasara kubwa.
Baadhi ya wakulima
hao ambao sasa wanatumia mabonde yaliomo
ndani ya wilaya hiyo kulima mazao hayo kama mazao mbadala ya biashara na chakula wamemueleza mkuu wa
wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe kuwa hatua hiyo ya kuachana na kilimo cha
pamba imetokana na hasara kubwa ambayo wameipata katika msimu wa mwaka jana wa zao
hilo.
Walisema
mbali na kutumia fedha nyingi katika kilimo cha zao la pamba lakini pia Serikali imeshindwa kuwapa mikopo ya zana za kisasa za kilimo kwaajili ya
kilimo cha pamba jambo ambalo limewafanya kuachana na kilimo hicho hivyo kuelekeza
nguvu zao katika kilimo cha mpunga na mahindi kwa kutumia jembe la mkono.
''Inakuwa haina maana ya kuendelea na kilimo cha zao hili kwani hakina manufaa kwetu tunatumia fedha nyingi katika kilimo hadi nyakani za mavuno lakini thamani ya mauzo inakuwa haikidhi.
"Ni bora tuelekeze nguvu zetu katika kilimo cha mazo mengine na pale
Serikali
itakapoona faida ya kilimo cha pamba kwa ajili ya masrahi yetu na Taifa
wataangalia namna ya kuwezesha hili,"walisema wakulima hao.
Hata hivyo
mkaguzi wa pamba wilaya ya Bunda Bw Igoro Marongo,pamoja na kuwapongeza
wananchi hao kufikiria kutafuta mazao mbadala lakini hatua hiyo isiwafanye
kutoachana na kilimo cha pamba badala yake walime kwa kufuata ushauri wa kitaalamu ili kuwawezesha kuzalisha zaidi ya
kilo 1,000 kwa ekari ili kupata fedha nyingi tofauti na hivi sasa.
"Ushauri wangu ni kuwataka wakulima wasiachane na
zao la pamba bali walime kitaalmu zaidi ili kupata mavuno kwa asilimia
kubwa ambayo itawezesha kupata fedha nyingi,"alisema Igoro.
Kwa sababu
hiyo Mkuu wa Wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe,ambaye aliwatembelea wakulima
hao katika kujionea kilimo hicho,amewaagiza maafisa kilimo katika ngazi ya Kata
na Wilaya kuhamasisha wakulima kuunda vikundi
ambavyo vitawawezesha kupata matrekta ya
kiliomo kutoka kwa makampuni makubwa yaliopo ndani ya wilaya hiyo.
Baadhi ya
mabonde ambayo yametangazwa na Mkuu wa Wilaya hiyo yatumike kwa kilimo hicho ni
pamoja na Nansimo,Mwitende,Igundu,Iramba,Namuhura pamoja na Karukekere,Bitaraguru,Mranda,Chingurubira
na Chamtigiti.
Post a Comment
0 comments