0
WANAJESHI WA MALI


Jeshi la Mali limewaua “kiholela watu kadhaa” katika harakati za kujaribu kuteka tena eneo la kaskazini lililoko chini ya mamlaka ya wapiganaji wa Waisilamu. 

Hii ni kwa mujibu wa kikundi cha kutetea haki za binadamu.
Shirikisho la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu, FIDH, limesema kwamba watu kadhaa waliuwawa kwa ajili tu walikuwa hawana vitambulisho.
Lakini mwanajeshi mmoja wa Mali alinukuliwa akikanusha madai hayo.

Madai mengine kuhusu mauaji ya kiholela pia yameripotiwa katika maeneo mengine ya magharibi na kati mwa nchi hiyo.
Wanajeshi wa Mali wapiaga doria mjini Diabali

Habari zinazosema kwamba jeshi hilo, ambalo wengi wao ni Waafrika weusi kutoka kusini mwa nchi, wamekuwa wakiwalenga Waarabu na Watuareg kutoka kaskazini, jambo linaloashiria ubaguzi wa rangi katika mapigano hayo, ubaguzi ambao umefichwa na kuwepo kwa vikosi kutoka nchi za magharibi wanaopambana na wanamgambo Kiisilamu.

Wakimbizi walioko kambini mjini Sevare

 
          CHANZO bbc swahili

Post a Comment