0








KIKOSI cha timu ya soka ya Waandishi wa Habari mkoani Mara Habari fc kimeanza mazoezi kwa ajili ya bonanza la Waandishi litakalofanyika siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari (Media Day) mey 3 katika viwanja vya posta Mjini Musoma.

Akizungumzia bonanza hilo,Mratibu wa bonanza George Marato alisema tayari maandalizi yanaendelea vizuri katika kufanikisha bonanza hilo ambalo litawashirikisha wadau mbalimbali wa Habari kwa lengo la kufahamiana na kujenga mahusiano.

Alisema mazoezi wameamua yaanze mapema katika mchezo wa mpira wa miguu ili kuandaa kikosi ambacho kitaendeleza rekodi ya kutokufungwa na timu yoyote tangu ilipoanzishwa na kutamba kuendelea na wimbi la kushinda katika michezo ambayo wanakutana na kila timu wanayokutana nayo.

Marato alisema bado wana kikosi kizuri cha timu ya mpira wa miguu licha ya kuwakosa kikosini wachezaji wao wawili Mabere Makubi na Cales Katemana ambao wameamia katika mikoa mingine ya vituo vipya vya kazi lakini wanaamini kuendeleza rekodi hiyo ya ushindi katika bonanza hilo.

"Katika bonanza hilli licha ya mchezo wa soka tutakuwa na michezo mingine kama riadha,kuvuta kamba,kukimbia kwenye magunia pamoja na kufukuza kuku yote haya tunayafanyia maandalizi na tunawashirikisha wadau mbalimbali katika kufanikisha siku hii ambayo itawakutanisha Waandishi wote wa mkoa wa Mara pamoja.

"Kwenye mpira wa miguu tumepanga kucheza na timu ya wakusanya kodi wa TRA Mara maana tuliwafunga na kuchukua kombe walioandaa wenyewe katika siku ya mlipa kodi sasa tunataka tuwadhihilishie kuwa hatukubahatisha pale tulipowafunga kwenye mchezo huo,"alisema Marato.

Mratibu huyo wa bonanza la Waandishi wa Habari alisema kabla ya kufanyika kwa bonanza hilo watakutana na wadau wa soka pamoja na michezo mbalimbali ili kuona namna ya kusaidiana na kurudisha hamasa ya michezo katika Manispaa ya Musoma pamoja na mkoa wa Mara kwa ujumla.

Alidai hamasa ya michezo imepungua tofauti na zamani na kwa sasa michezo imekuwa ikifanyika kwenye ligi za soka na inapomalizika wachezaji wanakaa mwaka mzima bila kufanya michezzo hivyo kuendelea kudumaza michezo ambayo kwa sasa imekuwa ni sehemu ya ajira na kujiongezea kipato.

Post a Comment