0


         






MBUNGE wa jimbo la Musoma Mjini Vicent Nyerere (CHADEMA) ametoa msaada wa mifuko mitano ya saruji kwa ajili ya kufanyia ukarabati choo cha msikiti wa Rahman Nyakato katika Maniuspaa ya Musoma ambacho kimearibika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Mkoani Mara.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Mbunge,Katibu wa Mbunge Fikiri Malenge alisema viongozi wa msikiti huo walifika katika ofisi ya Mbunge na kuomba msaada huo kutokana na kuharibiwa kwa choo hicho baada ya mvua ambazo zilifululiza katika kipindi cha hivi karibuni.

Alisema kutokana na umuhimu wa suala hilo Mbunge aliamua kutoa msaada huo kwa ajili ya kuanza kukarabati choo hicho ili waumini waendelee kufanya ibada bila kuwa na kikwazo pale inapoihitajika huduma ya choo.

"Kama tunavyofahamu Mbunge kwa sasa yupo kwenye vikao vya Bunge la Bajeti kule Dodoma lakini baada ya kupata taarifa hizi ameanza na msaada wa mifuko hii ya saruji lakini ameahidi kuendelea kusaidia ili ukarabati huu uweze kukamilika haraka na atakapotoa maelekezo mengine tutawasiliana na viongozi wa Msikiti,"alisema Fikiri.

Katibu huyo wa Mbunge alisema Uongozi wa Msikiti wa Rahman katika kukamilisha ukarabati wa choo hicho licha ya kuhitaji saruji pia kunahitajika vifaa mbalimbali vya ujenzi ili kuweza kukamilisha choo hicho ambapo Mbunge Nyerere ameahidi kuwa na mawasiliano na uongozi wa msikiti ili kukamilisha suala hilo.

Akipokea mifuko hiyo ya saruji,Katibu wa Msikiti huo Ustadh Iddy Ndimila alimshukuru Mbunge Nyerere kwa kuwa mtu wa kwanza kuona umuhimu wa suala hilo na kuchangia katika kuanza kukarabati choo hicho kilichoaribiwa na mvua.

Alisema Nyerere ameonyesha njia ya kusaidia kukamilisha suala hili lakini bado kuna mahitaji zaidi yanayohitajika hivyo kumuomba kila mmoja kuweza kuguswa na jambo hilo na kufika katika msikiti huo na kusaidia sehemu ya mahitaji yanayohitajika.

"Bado tunauhitaji wa mchanga,tofari,mbao na vifaa vingine vya ujenzi yoyote anaweza kusaidia na kila atakayetoa katika hili malipo yake tunayakabidhi kwa mola na msaada wake anaweza kuuleta pale msikitini Nyakato ama akapeleka katika msikiti mkuu wa Ijumaa na utatufikia,"alisema Ustadh Iddy.

Post a Comment