MTU mmoja mkazi wa kata ya Nyamatare Manispaa ya Musoma John Katute
(56),amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mara
akituhumiwa kwa kosa la kuharibu miundombinu ya maji ya Mamlaka ya Maji
Safi na Maji Taka Musoma (MUWASA) na kusababisha usumbufu kwa
watumiaji.
Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Faisal
Kahamba,imedaiwa na mwendesha mashitaka wa Mahakama hiyo Jonas Kaijage
mtuhumiwa alifanya kosa hilo katika maeneo hayo ya Nyamatare tarehe 13
machi 2013.
Mahakama ilielezwa na mwendesha mashitaka
huyo,mtuhumiwa amefanya kosa hilo kinyume na kifungu namba 47 kifungu
kidogo cha (1) na (2) ya sheria ya usambazaji wa maji namba 12 ya mwaka
2009.
Kaijage ameiambia Mahakama upelelezi wa kesi
hiyo bado haujakamilika ili mtuhumiwa wa kosa hilo la kuharibu
miundombinu ya usambazaji wa maji katika Manispaa ya Musoma ianze
kusikilizwa.
Mtuhumiwa wa kosa hilo yuko nje kwa dhamana ya watu
wawili kwa kiasi cha shilingi milioni mbili kila mmoja huku kesi hiyo
ikipangwa kusikilizwa tena aprili 30.
Home
»
»Unlabelled
» KIZIMBANI KWA KUHARIBU MIUNDOMBINU YA MAJI MUSOMA
Post a Comment
0 comments