0
Taasisi ya kifedha isiyokuwa ya kiserikali inayojishughulisha na mikopo Finca Tanzania Tawi la Musoma imesema kutokana na tatizo la ajira hapa Nchini Watanzania wanayo nafasi ya kukopa na kufanya ujasiliamali ambao utawaongezea kipato na kuendesha maisha ya kila siku.

Akizungumza na BLOG HII ofisini kwake,Meneja Wa Finca tawi la Musoma Patrick Swenya alisema bado kuna nafasi ya kujiajili kwa mtu yeyote kupitia ujasiliamali kwa kuchukua mikopo katika taasisi za kifedha na kuendesha biashara mbalimbali.

Alisema Finca kwa sasa imeongeza wigo wa huduma zake hapa Nchini kupitia matawi mbalimbali ambayo yanawawezesha Wananchi kuchukua mikopo na kuendesha biashara ambazo zinaweza kupunguza kasi ya ukali wa maisha.

Swenya alisema Finca ili kuhakikisha Wananchi wanaochukua mikopo katika taasisi hiyo wananufaika nayo ina utaratibu wa kuendesha mafunzo ya ujasiliamali na biashara kutoka kwa maofisa wake kwa wahitaji wa mkopo kabla ya kuwapa mikopo hiyo.

Alisema kutokana na tatizo la ajira kwa sasa hapa Nchini,amewaomba  Vijana wanaotoka vyuoni kuacha kutegemea ajira za Serikalini bali wanaweza kuendesha maisha kwa kujiajili kwa kufanya biashara kutokana na kuchukua mikopo katika taasisi za fedha.

"Vijana wengi wanaohitimu masomo vyuoni kila mmoja anataka aajiliwe Serikalini hili haliwezekani maana tunashuhudia ajira zilivyo chache hapa Nchini hivyo hakuna budi kuwa wajasiliamali kwa kutafuta fedha katika taasisi za fedha ili wajikomboe,"alisema Swenya.

Alidai Finca bado inayo nafasi kwa mtu yoyote anayehitaji kujiajili kwa kuchukua mkopo na kufanya biashara kujiunga katika vikundi ama mtu binafsi milango bado ipo wazi katka taasisi hiyo hivyo fursa  itumiwe katika kujiletea Maendeleo.

Akizungumzia uanzishwaji wa huduma za kibenki katika taasisi hiyo Makao Makuu Jijini Dar es salaam,Meneja wa Finca tawi la Musoma alisema huduma hiyo kwa sasa inatolewa katika matawi yake matatu Jijini humo na utaratibu unaendelea kufanyika ili huduma hizo za kibenki ziweze kufanyika katika matawi mengine.
                      

Post a Comment