KATIBU
Mkuu wa Mabingwa wa Soka Tanzania Bara, Yanga ya jijini Dar es Salaam,
Lawrence Mwalusako, leo amemtambulisha rasmi Mshambuliaji mwenye
mapenzi ya moyoni na timu hiyo Mrisho Ngassa, aliyekuwa na mahasimu wao
wakuu, Simba.
Mwalusako,
amemtambulisha Ngassa kuwa hivi sasa ni mchezaji mpya na halali wa
Yanga, baada ya kuanguka saini ya kuitumikia Klabu hiyo kwa miaka
miwili, ili kuisaidia katika msimu ujao wa Ligi kuu ya Tanzania Bara na
michuano ya kimataifa, inayoikabili timu hiyo baada ya kuwa mabingwa na
Ligi Kuu iliyomalizika jana.
Ngassa, ameamua
kurudi Yanga baada ya kuihama timu hiyo na kutimkia, Azam FC na baade
kabla ya mwaka jana kuuzwa kwa mkopo, Simba, ambako amekuwa akisumbuliwa
kila mara na viongozi hadi mashabiki kuwa hana mapenzi na timu hiyo na
hasa kwa kitendo chake cha kubusu Jezi ya Yanga aliyorushiwa na mmoja wa
mashabiki wa Yanga, katika moja ya mechi za mwaka jana wakati akiwa
Azam.
Aidha
Mwalusako, alisema kuwa Ngassa, ni mchezaji wa kwanza kutangazwa na
klabu hiyo na kusani mkataba wa miaka miwili ikiwa ni muda mfupi tu
baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu, ambapo ni leo ni siku muhimu iliyokuwa
ikisubiriwa na Viongozi wa Yanga, Ngassa na hata mashabiki wa Yanga,
waliokuwa wakiushauri uongozi kumrejesha Ngassa ''Tunduni''. na tayari
ameshaanguka saini ya kuichezea klabu yake hiyo ambayo anamapenzi nayo
makubwa hapa nchini kwa miaka 2.
Ngassa, akibusu Jezi ya Yanga, baada ya kukabidhiwa na Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako, wakati wa utambulisho rasmi uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. |
Post a Comment
0 comments