0

Hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo iliyokuwa ikisomwa na Msemaji (Waziri Kivuli wa Wizara hiyo) ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ Bungeni imesimamishwa kwa kile kilechoelezwa kukiuka taratibu za Bunge.

Akisimama kuomba Muongozo wa Spika, Mbunge wa CCM jimbo la Mbozi Mashariki, Godfrey Weston Zambi, aliliambia Bunge kuwa Hotuba hiyo katika kurasa zake 12 za awali imejaa maneno ya uchochezi kwa Serikali ya CCM.

Zambi alisema miongoni mwa maneno hayo ya Uchochezi ni yale ya kusema kuwa Serikali ya CCM kuwashambulia wanahabari kwa kuwapiga, kuwang’oa kucha, kuwamwagia tindi kali na kuwaua jambo ambalo sio kweli.

Kufuatia hatua hiyo Spika wa Bunge Anne Makinda alipokea Mwongozo huo na kuliahirisha Bunge hadi Hotuba hiyo itakapo pitiwa upya ndipo iletwe tena Bunge hapo.

Post a Comment