MKAZI wa kata ya Nyakato katika Manispaa ya Musoma Msafiri Antony (34)
aliyeachiwa na Msamaha wa Rais aprili 26 mwaka huu katika sherehe za
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar amekamatwa na jeshi la polisi mkoani
Mara baada ya kukutwa na marobota 2 ya nguo za kike pamoja na majola 10
ya vitambaa vya kike vinavyodaiwa kuwa vya wizi.
Akizungumza na
waandishi wa Habari ofisini kwake,Kaimu kamanda wa polisi mkoani Mara
Afisa Mnadhimu wa polisi Paul Kasabago alisema mtuhumiwa huyo
al;ikamatwa alikamatwa mei 20
akiwa katika gari namba T 974 CED Toyota Hiace ikitokea Bunda kwenda
Musoma baada ya kupata taarifa kutoka kwa Wananchi wema.
Kasabago
alisema mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa akitumikia kifungo kutokana na
kosa la kuvunja nyumba
usiku na kuiba kabla ya kuachiwa na Rais alikuwa miongoni mwa
washitakiwa wengine wawili ambao walikamatwa siku hiyo wakiwa katika
gari lingine lenye namba T 547 BSF Toyota Hiace ambayo pia ilikuwa
ikitoka Bunda kwenda Musoma wakiwa na bunduki aina ya S/Gun
iliyotengenezwa kienyeji na risasi 3.
Kaimu kamanda huyo
aliwataja watu hao ambao pia walikutwa na mafurushi 4 ya nguo mbalimbali
pamoja na Tv inchi 14 kuwa ni Mwita Mkama (40)mkazi wa Tarime pamoja na
Catherine Sinza (28) mkazi wa Bunda ambaye baada ya kupekuliwa maungoni
mwake alikutwa na risasi 3 ndani ya chupi aliyokuwa amevaa.
"Watu
hawa walikuwa kitu kimoja na walikuwa wamepanda magari hayo tofauti ili
kuweza kufanikiwa kufika kule walikokuwa wakienda lakini kutokana na
ushirikiano wa Wananchi kwa kutoa taarifa za siri tulifanikiwa kuweka
mitego na kuwakamata na hadi sasa bado tunaendelea kuwachua maelezo na
pale upelelezi utakapokamilika tutawafikisha
mahakamani.
"Tunawaomba Wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa
jeshi la polisi ili kuweza kukomesha watu wote ambao wanajihusisha
katika vitendo vya kiuhalifu katika makazi kwa kuwa hawa wanaofanya
vitendo hivi wanakaa huko na wengine wanafahamika na jeshi la polisi
haliwezi kutoa siri kwa mtoa taarifa,"alisema Kasabago.
Aidha
kaimu kamanda wa polisi mkoani Mara alisema katika oparesheni ambayo
inaendelea katika maeneo mbalimbali walifanikiwa kumkamata mtu mmoja
Adamu Maiga (30 anayetuhumiwa kutenda kosa la mauaji aprili mosi katika
Supermarket ya Cotra iliyopo Baruti katika Manispaa ya Musoma.
Katika
oparesheni hiyo walikamatwa watu watatu kuhusiana na makosa ya
unyang'anyi wa kutumia siraha kwenye maeneo mbalimbali Wilayani Bunda
ambao bado wanaendelea kuhojiwa na jeshi la polisi na baada ya kukamilka
kwa upelelezi watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili.
Home
»
»Unlabelled
» ALIYEACHIWA NA RAIS KWA MSAMAHA AIBA TENA
Post a Comment
0 comments