SERIKALI inakusudia kuboresha huduma ya maji ili wananchi mkoani Mara
waweze kupata huduma hiyo kwa uhakika na kuondoa kero ambazo mbalimbali za huduma hiyo ikiwemo umbali wa kupata maji.
Hayo yalisemwa na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe akiwa katika
ziara ya siku tatu mkoani humo katika kukagua miradi mbalimbali ya maji.
Alisema Serikali imekusudia kutumia sh.bilioni 1.1 kuboresha
huduma hiyo kwa kurekebisha na kununua pampu mpya kwa kuweka vioski 30 na miradi
kutengenezwa upya kwa kulingana na watu
ili maji yaweze kuwafikia wananchi kwenye maeneo yao.
Waziri Maghembe alisema Wizara ya maji itatumia jumla
ya shilingi Bilioni 300 katika
kutekeleza miradi wa huduma ya maji katika mikoa mitatu ya Bukoba ,Mwanza na
Mara .
Alisema
maeneo ya miradi hiyo ya maji yamesha andaliwa kutokana na mazingira ya
mikoa hiyo lengo likiwa kuondoa kero ambazo wanazipata Wananchi
kutokana na upatikanaji wa maji.
”Tayari Wizara yangu imekubaliana na Benki ya Maendeleo na kusaini kuchukua mkopo wa shilingi bilioni 25
ili kuboresha mradi wa Mgango uliopo wilaya ya Butiama ambapo katika mradi
wa chanzo kipya cha Bukanga wa wilaya
ya Musoma utagharimu shilingi bilioni 80 ”,alisema
Maghembe.
Alisema ifikapo mwezi Julai Wizara
itakuwa imeleta wataalam ambao
wataangaalia namna ujenzi wa mIradi hiyo
ili kuweza kudumu kwa muda mrefu zaidi
na kufikia miaka 20 kwa mujibu wa
utekelezaji wa ilani ya Chama cha mapinduzi.
Maghembe aliwataka Wananchi kutoa ushirikiano kwa wataalam ili kuharakisha huduma hiyo inapaikana na kwamba wananchi hao
wakae mkao wa kupata huduma ya maji ya uhakika.
”Pale ambapo maji yanachukuliwa na
kupita ni lazima watu wa eneo hilo wapate maji ili waweze kusaidia kulinda mradi husika ili wale wasio wazalendo na waharibifu wa miundombinu wasiihujumu”aliongeza.
Akiwa katika Wilaya ya Butiama,Waziri Maghembe alipokea kero za Wananchi kupitia Afisa Mtendaji wa Kata ya Butiama
Raphael Kakwaya alizitaja kero
zinazosababisha wananchi
kutokupata maji wilayani humo ni mitambo chavu, baadhi ya watu wanapata huduma hiyo kuwauzia maji kwa bei ya
juu kuanzia shilingi 150 hadi 200 kwa
ndoo ya lita 20 na na wafanyakazi wa
Mugango-Kiabakari na Butiama kutolipwa mishahara yao tangu mwaka 2011 na hivyo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi .
Waziri wa
maji Profesa Maghembe katika ziara yake mkoani Mara lengo ni kutembelea na
kukagua miradi ya maji kwa kukagua mradi wa Chanzo kipya cha Bukanga katika wilaya Musoma, mradi wa
maji wa Mugango ,Butiama pamoja na kukagua mradi wa bwawa la Manchira Wilayani Serengeti.
Post a Comment
0 comments