TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Mara
imeendelea kuzifatilia taasisi mbalimbali za Umma kuhusiana na matumizi
mabaya ya Mamlaka huku safari hii ikiwaburuza Mahakamani waliokuwa
watumishi wa Idara ya Afya katika Manispaa ya Musoma.
Watumishi
waliofikishwa Mahakamani aliyekuwa Mkuu wa Idara ya afya katika Manispaa
hiyo Charles Mkombachepa pamoja na aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Idara hiyo
Melinda Chafora ambao wamefunguliwa shitaka la Uhujumu
uchumi namba 03 ya mwaka 2013 kwa makosa ya matumizi mabaya ya Mamlaka
kinyume na kifungu cha 31cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwanamba 11/2007 na kosa la kuisababishia hasara Serikali.
Hata
hivyo aliyesomewa mashitaka ni
mshitakiwa wa kwanza Melinda Chafora ambapo mshitakiwa pili hakuweza
kufika Mahakamani na kuandikiwa hati ya mshitakiwa kufika Mahakamani
juni 26 2013 ili asomewe mashitaka yake.
Mshitakiwa wa kwanza
amesomewa mashitaka na Mwendesha mashitaka wa Takukuru Erick Kiwia mbele
ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mara Emanuel Ngigwana
ambapo mshitakiwa amekana mashitaka na kuachiwa kwa dhamana.
Mwendesha
mashitaka wa Takukuru alisema kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na
Takukuru umebaini Melinda Chafora akiwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Afya ya
Manispaa ya musoma kuanzia tarehe 15/10/2007 alitumia mamlaka yake
vibaya kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake kulikopelekea watumishi
wanne ambao ajira zao zilikoma kwa kustafu na kufariki kujipatia malipo
ya mishahara isiyo halali.
Alidai watu hao walijipatia kiasi cha
shilingi 1,692,160.32 kwa kipindi cha mwezi julai hadi oktoba mwaka 2008
kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Alieleza kutokana
na matumizi hayo mabaya ya mamlaka aliisababishia Serikali hasara ya
shilingi 1,692,160.32 kinyume na aya ya 10 (1) kifungu cha 57 (1) cha
jedwali la kwanza la Sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 200 kama
ilivyofanyiwa mapitio mwaka 2002 kwa kufanya uzembe na kutokuwa makini
katika kutekeleza majukumu ya kuwaondoa watumishi hao katika (payroll)
za mwezi julai,agosti,septemba na okotoba mwaka 2008.
Aliongeza
uchunguzi pia ulibaini mshitakiwa wa pili Charles Mkombachepa akiwa Mkuu
wa Idara ya Afya katika Manispaa ya Musoma alitumia mamlaka yake vibaya
wakati akitekeleza majukumu yake na kupelekea watumishi hao kujipatia
mishahara hewa jumla ya shilingi 947,232.52 kwa miezi ya novemba na
desemba 2008 kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana
na Rushwa namba 11/2007
Home
»
»Unlabelled
» TAKUKURU MARA YANASA WATUMISHI WENGINE KWA KUIDHINISHA MISHAHARA HEWA
Post a Comment
0 comments