0
HALIMASHAURI ya Wilaya ya Butiama imevuta kasi katika kampeni ya kuchangia damu iliyoanza aprili 15 ikiwa na lengo la kuokoa vifo vya mama wajawazito pamoja na watoto wachanga wakati wa kujifungua.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uchangiaji wa damu uliofanyika katika viwanja vya mwenge Wilayani hapa,Makamu Mwenyekiti wa Halimashauri ya Wilaya ya Musoma Denis Ekwabi alisema hadi kufikia sasa tayari zimekwisha kusanywa chupa za damu 871 kutoka kwa Wananchi waliojitolea.

Alisema kiasi hicho cha damu kimekusanywa kutokana na uhamasishaji uliofanywa na timu ya wakusanya damu kutoka Idara ya afya chini ya Mganga mkuu wa Wilaya Gencwele Makenge kwa kupita katika maeneo mbalimbali ya Wilaya.

Ekwabi alisema Wananchi wa Wilaya ya Butiama wameitikia wito wa uchangiaji wa damu kutokana na kuelewa namna ambavyo vifo vya mama wajawazito pamoja na watoto wachanga vinatokea wakati wa kujifungua huku tatizo kubwa linalosababisha vifo hivyo likiwa ni damu.

Alisema kiasi cha chupa 871 za damu ambazo zimekusanywa hadi sasa ni zaidi ya lengo ambalo limewekwa na mkoa wa Mara kukusanya chupa 600 kwa kila Wilaya itakapofikia juni 14 siku ya maazimisho ya uchangiaji damu anbapo kitaifa itafanyika mkoani Mara.

Aidha Ekwabi ameendelea kutoa wito kwa Wananchi wa Wilaya ya Butiama kuendelea kuchangia damu kwa kuwa hitaji la damu halina kikomo hivyo kushilikiana na timu ya ukusanyaji damu ili kupata chupa nyingi zaidi kutoka kwa wale wenye sifa za kutoa.

 Awali mkurugenzi wa Shirika la (Evidence For Action) Craig Ferla linaloshughulika na kampeni ya uchangiaji wa damu Tanzania alisema vifo vya akina mama na watoto wachanga wakati wa kujifungua ni vingi hapa Nchini kuliko sehemu nyingine Duniani hivyo wanaweza kuokolewa kwa kuchangia damu.

Alisema kiasi cha chupa 450,000 za damu zinahitajika kwa mwaka Nchini Tanzania huku kiasi kikubwa kikitumika kuokoa maisha ya mama na watoto lakini cha kusikitisha chupa 150,000 za damu ndizo zinazopatikana na kusambazwa hivyo jitihada zaidi zinahitajika katika kuchangia.

"Kiwango kikubwa cha uhaba wa damu kinapelekea akina mama wengi kufa,takwimu zinaonyesha kina mama 48,000 na watoto 8,000 ufariki dunia kutokana na upungufu wa damu hapa Tanzania,kiwango hiki ni kikubwa hivyo lazima tushirikiane kuokoa hali hii.

"Akina mama na watoto wachanga ufariki dunia kutokana na hali hii,ni lazima kwa pamoja tuhakikishe vituo vya tiba vitoe huduma stahiki kwa mama zetu na watoto wachanga ili kuwaokoa,"alisema Craig.

Post a Comment