0




MBUNGE WA JIMBO LA RORYA LAMECK AIRO AKIKAGUA UJENZI WA MRADI WA BWAWA LA MAJI KATIKA KIJIJI CHA OSIRI KATA YA ROCHE


Wananchi wa Kijiji cha Osiri kilichopo Kata ya Roche wilayani Rorya wanalazimika kwenda maeneo ya Nchi jirani ya kenya kwa ajili ya kupata huduma ya maji kwa mahitaji mbalimbali hali iliyowafanya kumuomba Mbunge wa jimbo hilo Lameck Airo kusaidia kukamilika kwa mradi wa maji wa Tasaf ulioanzishwa kijijini hapo.

Hayo wameeleza mbele ya Mbunge huyo alipokuwa akikagua miradi mbalimbali ya Maendeleo katika Jimbo la Rorya na kudai kutokana na uhaba wa maji kunawapelekea kuvuka mipaka hadi Nchini kenya kwa ajili ya kupata maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu pamoja na wanyama.

Walisema tatizo la maji katika kijiji hicho na vijiji vingine vitatu vilivyopo Kata ya Roche  kunawasababishia kuishi katika mazingira magumu ya kukosa huduma hiyo ikiwemo kwa binadamu pamoja na wanyama wanaowafunga.

Wananchi hao waliishukuru Serikali kwa kuwapatia mradi wa bwawa la maji kupitia mradi wa Tasaf lakini wakaomba nguvu ya Mbunge wa Jimbo hilo ili uweze kukamilika kwa haraka na ufanisi zaidi ili kuondokana na adha hiyo.

"Tunaishukuru sana Serikali kwa mradi huu wa maji hapa Osiri kwani tuna matatizo makubwa sana lakini kutokana na nguvu zetu pia tunaomba na nguvu za Mbunge wetu ili mradi huu ukamilike mapema nasi tupate maji.

"Kwa sasa tunalazimika kwenda kupata huduma ya maji Nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya matumizi ya binadamu pamoja na mifugo yetu na sio karibu na hapa kijijini hivyo tunaangaika kupata huduma hiyo,"alisema Onyango Samwer.

Akizungumza mara baada ya kuangalia mradi huo,Mbunge wa jimbo la Rorya Lameck Airo alisema atakuwa bega kwa bega kuhakikisha mradi huo unakamilka kwa kuweka nguvu zake na kuongeza vifaa ili uweze kukamilika.






Alisema amewasiliana na mkandarasi wa Halimashauri na kumtaka wakandarasi waliopo katika eneo la mradi waweze kukaa eneo hilo hadi mradi utakapokamilika na yupo tayari kughalamikia ziada ya mradi huo.

"Nimeagiza maroli yangu yaje hapa na yatafika hapa ili kuweza kusaidia shughuli za hapa na maji yaweze kupatikana ili adha ya matatizo ya maji mliyonayo yaweze kukamilika kwa muda muafaka.

"Naomba nanyi Wananchi muwape ushirikiano wakandarasi kwa kile watakachowaleza ili mradi huu usije kuaribika kwa kuingilia eneo la mradi kwa kilimo na shughuli nyingine ambazo zitakwamisha,"alisema Lameck.

Post a Comment