0
MZEE mmoja (80) Benedicto Marwa mkazi wa Kitongoji cha Mashine ya maji kata ya Bunda Stoo mjini Bunda Mkoani Mara amelalamika nyumba zake kubomolewa na kutishiwa kupelekwa polisi kwa kudai fidia ya mali zake kutoka kwa idara ya ardhi wilayani Bunda licha ya ofisi ya Waziri Mkuu kutoa barua ya kufatilia suala lake lakini imekuwa kimya.
 
Akitoa malalamiko yake hivi karibuni kwa Waandishi wa Habari Mjini Bunda,Marwa alidai licha ya kuwasilisha malalamiko yake kwa wakati tofauti katika ofisi mbalimbali za serikali bado maofisa wa aridhi waliovamia maeneo yake wameendelea kuyashikilia huku wakiwa wamejenga nyumba zao na kukahidi maelekezo yaliyotolewa.
 
Alitaja ofisi alizowahi kuwasilisha kero zake kuwa pamoja na  Ofisi ya mkuu wilaya ya Bunda, Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mara, Baraza la ardhi, nyumba na Makazi mkoani Mara na Kamishna ya Ardhi Wizarani lakini bado maamuzi hayafanyiwi kazi huku akiendelea kuangaika kuitafuta haki yake ya kurudishiwa maeneo.
 
Akionesha vielelezo  kwa Wandishi wa Habari, alisema Mahakama ya Ardhi, Nyumba na Makazi ya wilaya ya Musoma  mkoani Mara ilihukumu kesi hiyo MISC Application No.85 ya mwaka 2010, kwa kutoa siku 30 kwa maofisa wa ardhi kumrejeshea eneo lake katika Kitongoji cha mashine ya maji mjini humo.
 
Alisema agizo lilitolewa Novemba 5, 2010 ambapo Kampuni ya UBAPA LTD and Tribunal Broker ilitakiwa  kubomoa nyumba zilizojengwa katika eneo lake lakini anashangazwa na kampuni kuendelea kuwa na kigugumizi cha kutekeleza agizo lililotolewa huku akidai huenda kampuni hiyo inashindwa kufanya hivyo kwa kuwa inategemea kazi nyingi kutoka katika idara ya ardhi ya Bunda.
 
Vielelezo vimebaini kuwa hiyo ni hukumu ya pili ambapo hukumu ya kwanza ya kurejeshewa eneo lake lilitolewa na Baraza la ardhi la Kata ya Bunda Na.77 mwaka 2009 lakini Ofisa ardhi ya wilaya ya Bunda wakati huo (jina tunalo ) hakuridhika na kukata rufaa kuhamisha hukumu hiyo kwenda mahakama ya ardhi nyumba na makazi wilayani Musoma.
 
Kutokana na hatua hiyo April 4, mwaka huu Mahakama ya Ardhi Nyumba na Makazi Musoma iliagiza Kampuni ya UBAPA and TRIBUNAL BROKER kutekeleza agizo la Mahakama hiyo Na.85 ya mwaka 2010.
 
 Marwa alidai  kwamba kwa  muda huo wote, maofisa hao wanatumia fedha ili agizo la mahakama hiyo isitekelezwe huku wakiendeleza eneo hilo licha ya kuzuiliwa na  badala yake waliamua kumfikisha  polisi kuwa ni mvamizi na kudai anasikitishwa na na anavyofanyiwa licha ya kuwa na umri mkubwa na kuviomba vyombo vya juu kumsaidia kuipata haki yake ambayo anadai vielelezo vyote anavyo huku akikabidhi nakala ya vielelezo hivyo katika Gazeti hili ikiwemo barua kutoka ofisi ya Waziri Mkuu.
 

Post a Comment