0
 







 
MKUU wa mkoa wa Mara John Tupa amewahimiza viongozi kuanzia ngazi za Kata,Wilaya na mkoa kuhakikisha wanasimamia na kuwa na ufatiliaji wa karibu kuhakikisha mifugo inaogeshwa ili kuweza kuepukana na magonjwa yanayotokana na kupe na kusababisha vifo vya mifugo.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa kikao cha majumuisho ya mradi wa ufufuaji wa majosho ya kuogeshea ng'ombe uliofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uholanzi (SNV) kwa kushirikiana na wadau wa mifugo mkoani Mara.

Amesema kazi kubwa iliyofanywa na SNV na wadau wa mifugo kwa kufatilia ufufuaji wa majosho kwa lengo la kuhakikisha mifugo inaogeshwa inafaa kuenziwa kwa viongozi kutoa elimu kwa wafuagaji nakuona umuhimu wa kuogesha mifugo ili kuwaepusha na magonjwa yaenezwayo na kupe.

Tupa ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho amesema mkoa wa Mara ambao una mifugo mingi zikiwemo ng'omb zaidi ya milioni moja ambayo Wananchi wamekuwa wakitumia kama uchumi,chakula na mahitaji mengine inafaa wafugaji wapate elimu ya kutosha namna ya kufuga kwa tija na utamaduni wa kuosha mifugo.

Amesema kila Wilaya lazima ijue uhitaji wa majosho katika maeneo yao na kutumia ongezeko kubwa la majosho lililopo kutokana na kazi iliyofanywa na SNV na wadau wa mifugo wafugaji waweze kuogesha mifugo na kutokomeza vifo ambavyo ni zaidi ya asilimia 70 vinavyotokana na ugonjwa unaosababishwa na kupe.

 Akichangia katika kikao hicho ambacho pia kiliwahusisha wakuu wa wilaya,wakurugenzi na maafisa wa mifugo kutoka Wilaya zote za mkoa wa Mara,afisa mifugo wa Wilaya ya Bunda Maxmillian Marwa alisema Serikali iangalie upatikanaji wa dawa za ruzuku ili kukabiliana na changamoto ya majosho.

Amesema ruzuku ya dawa inayopatikana kwa mkoa wa Mara haiendani na idadi ya mifugo hivyo ni muhimu ruzuku hiyo ikaongezwa ili kuendana na hali halisi pamoja na Serikali ya mkoa wa Mara kuvumbua njia ya mifungo inapopita kwenda kuoshwa kutokana na maeneo mengine kuvamiwa na wakulima.

Kwa upande wake Meneja wa mradi wa mifugo kutoka Kanisa la Anglican dayosisis ya Mara (AIC-Mara)ambao walishirikiana na SNV dokta Theophil Kayombo amesema baada ya kutembelea mjosho katika kufatilia ufufuaji wamekutana na changamoto mbalimbali ikiwemo kutotekelezwa kwa sheria ndogo ndogo za ogeshwaji wa mifugo.

Amesema Serikali inapaswa kuweka mkazo katika uogeshaji wa mifugo kutokana na baadhi ya Wananchi kuwa na visingizio vingi pale wanaposhindwa kwenda kuogesha mifugo na kuwa na mawasiliano kutoka ngazi ya josho ili kuwza kufatilia uogeshaji.
 

Post a Comment