0
 
 

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Musoma Mjini kimejipanga kwa kuanza ziara ya kutembelea kata 13 za Wilaya hiyo kuwakumbusha viongozi na wanachama wake wajibu wao katika Chama lengo likiwa kujiimalisha na kuweka nguu ya pamoja kuhakikisha wanafanya kazi kwa pamoja ya kukijenga chama na kufanya vizuri katika uchaguzi wa Serikali za mitaa hapo mwakani na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Akizungumza na MTANZANIA mara baada ya kumalizika kwa ziara ya kutembelea kata hizo iliyoongozwa na Mjumbe wa Halimashauri Kuu ya CCM (NEC) Vedastus Mathayo,Katibu wa CCM Wilaya ya Musoma Mjini Musa Motoroka alisema ziara hiyo ni moja ya majukumu ya Chama katika kukumbushana wajibu na utendaji wa kazi.

Alisema ziara hiyo ilikuwa na mafanikio kwa kukutana na viongozi na wanachama wa kutosha na kuzungumza nao mambo mbalimbali ambayo yana lengo la kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisa kazi za Chama kuanzia ngazi za Tawi,Shina hadi Kata zinafanywa kwa ushirikiano kwa kusudio moja la kukijenga Chama.

Katibu huyo wa CCM alisema bila kuwa na vikao na kukumbushana wajibu wa majukumu ya kila mmoja kama Chama cha Siasa kazi haziwezi kwenda na kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu wake akiwa kiongozi ama mwanachama kwa kushiriki shughuli zote ikiwa katika Shina,Tawi ama Kata.

"Tumefanya ziara katika Kata zote 13 za Wilaya yetu ya Musoma Mjini na imekuwa na mafanikio makubwa  kwa kukutana na viongozi wote pamoja na wanachama na kupanga mambo mbalimbali na kuhimizana kila mmoja kutimiza wajibu wake akiwa mwanachama wa Chama cha Mapinduzi.

"Ziara hii sio ya kwanza,tunakutana na viongozi na wanachama wetu mara kwa mara katika kukumbushana wajibu,unajua mbeleni kuna uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa hiiyo siri kubwa ya ushindi ni kuwa pamoja na kufanya vikao na ndio maana tunafanya ziara katika kukumbushana wajibu,"alisema Motoroka.

Kwa upande wake Mjumbe wa Halimashauri Kuu ya CCM (NEC) Vedastus Mathayo alisema ahadi yake ya kuzifanya ofisi zote za CCM Musoma Mjini kuwa za kisasa kwa kuzitengeneza imeshaanza kwa kuwakumbusha viongozi wa Kata kuharakisha kutafuta maeneo ambayo yatajengwa ofisi hizo.

Alisema ahadi yake aliyoitoa katika uchaguzi ndani ya CCM ataitekeleza mara moja iwapo viongozi wa Kata watampelekea mapendekezo yao mahala ambapo wanataka ofisi yao ikae na kudai kuwa alitoa ahadi hiyo kwa kuamini shughuli za Chama zinapaswa kufanyika mahala ambapo ni pazuri na sahihi.

Post a Comment