0





TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoani Mara (TAKUKURU) inamshikiria  askari wa jeshi la polisi mkoani mara namba F.1863 Maridad David Kapinga wa kituo kikuu cha polisi mjini Musoma kwa kosa la kuomba na kupokea Rushwa ya shilingi elfu ishilini.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya Habari,Mkuu wa Takukukuru mkoa wa  Mara Holle Makungu alisema askari huyo mnamo septemba 10 mwaka huu alikamatwa na maafisa wa Taakukuru akipokea kiasi hicho cha fedha baada ya kumuomba kiasi hicho cha fedha Raia mwema na kutoa taarifa Takukuru.

Alisema askari huyo aliomba kiasi hicho cha fedha kutoka kwa mtu huyo baada ya kufatilia kitambulisho chake  cha mkazi alichomdhamini ndugu yake kama masharti ya dhamana aliyekuwa na tuhuma zilizofunguliwa katika kituo hicho kwa kumbukumbu RB/2818/2013.

Holle alisema baada ya kupokea taarifa hizo mtego uliwekwa ili kuweza kumnasa askari huyo ambapo maafisa wa Takukuru walifanikiwa kumkamata askari huyo maeneo ya Tanesco Musoma akiwa tayari ameshapokea kiasi hicho cha fedha.

Mkuu huyo wa Takukuru alisema uchunguzi dhidi ya tukio hilo bado unaendelea kufanywa na Taasisi hiyo na mara utakapokamilika hatua zaidi zitachukuliwa kwa askari huyo kwa mujibu wa sheria zinazozuia vitendo vya kuchukua na kupokea Rushwa.

Alisema askari pamoja na watumishi wa Umma  kwa ujumla wao wana kila sababu kuzingatia maadili ya kazi zao katika utekelezaji wa nyadhifa walizokabidhiwa na kuepukana na kuomba Rushwa kwani kufanya hivyo kunapelekea haki stahili kupotea na kukwamisha shughuli za kimaendeleo.

Aliongeza kuwa maafisa wa Takukuru wataendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuwafatlia wale wote wanaojihusisha na vitendo vya Rushwa na kudai kazi hiyo haiwezi kufanikiwa bila kuwa na ushirikiano baina ya  Wananchi na na wale wote wanaochukia vitendo vya Rushwa.

Aidha  Holle amewaasa Wananchi mkoni Mara kuendelea kutoa taarifa kwa taasisi hiyo ili kuweza kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea Rushwa vinavyofanywa na watumishi katika idara mbalimbali ambao sio waaminifu.

Post a Comment