0

WAMAMA WA LINE POLISI WAKISUBILI MKWANJA
MSIENDE KUSUKIA NYWELE ZA GHARAMA HIZI FEDHA!
MIJIERA LIVE!
TIA SAHIHI HAPA KABLA YA KUPOKEA TUSIJE KUGEUKANA,NI KAMA ANASEMA MTENDAJI WA MUKENDO
MWENYEKITI BI.MWAMVITA ADAMU AKIPOKEA FUNGU TOKA MWAKILISHI WA MBUNGE NYERERE DIWANI WA VITI MAALUMU BI.MARIAMU(CHADEMA)
NI FURAHA TUPU BAADA YA KUVUKA MKWANJA
KIKUNDI cha Wanawake wajasiliamali cha Mshikamano Line Polisi kilichopo katika Manispaa ya Musoma kimeupongeza uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini Vicenti Nyerere kwa kufatilia na kuhakikisha vikundi vya Wanawake na Vijana vinapata mikopo kwa ajili ya Maendeleo.


Wanawake hao walisema kwa zaidi ya miaka mitano ya nyuma tangu wamekuwa wakijishughulisha na ujasiliamali hawajawahi kupata mikopo kutoka Halimashauri ya Manispaa ya Musoma nah ii ni mara ya kwanza kuona wanatazamwa na kupata mikopo hiyo ambayo imedaiwa huwa inatoka kila wakati kupitia mfuko wa Maenmdeleo.


Kauli hiyo ilitolewa na Wanawake hao wanaoishi Kata ya Mukendo baada ya kukabidhiwa kiasi cha shilingi milioni mbili na laki tatu na Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini na Diwani wa Kata ya Mukendo Vicenti Nyerere (Chadema)ili kuongeza mitaji kwenye shughuli zao za ujasiliamali ikiwa ni mikopo ya gharama nafuu na kurudishwa kwa ajili ya kuwapa watu wengine.


Akizungumza mara baada ya kupokea kiasi hicho cha fedha,Mwenyekiti wa kikundi hicho chenye wanachama 20 Mwamvita Adamu, alishukuru kuona uongozi uliopo sasa kwenye Manispaa ya Musoma kufatilia na kuhakikisha vikundi vya ujasilimali vinapata mikopo nafuu inayotoka kwenye mfuko wa Maendeleo hivyo kubolesha na kuimalisha biashara zao.


Alisema mikopo waliyopata watahakikisha hawaiweki kwenye shughuli nyingine zaidi ya kuongeza mitaji ili kuweza kujiongezea kipato na kuweza kuirudisha ili watu wengi zaidi waweze kukopeshwa na kuondokanana wimbi la umasikini katika familia.


Mwenyekiti huyo alisema licha ya kusikia huwa kuna fedha kwenye Halimashauri zinazokopeshwa kwa gharama nafuu kwa vikundi vya Wanawake na Vijana lakini hawajawahi kupata fedha hizo na ni mara ya kwanza na kudai uongozi wa sasa uliopo unapaswa kupongezwa kwa hatua hiyo.


Akizungumza na Wanawake wa kikundi hicho kabla ya kutoa fedha hizo kwa niaba ya Mbunge,Diwani wa viti maalumu Mariamu Daud(Chadema) alisema fedha hizo zitatolewa kwa Kata zote 13 za Jimbo la Musoma na wameanza na Kata ya Mukendo na kusema fedha zote zitakazo husika na mikopo ya Wanawake na Vijana zinawafikia.


Alisema katika vikao walivyokaa vya Halimashauri ya Manispaa ya Musoma kwa kushirikiana na Mkurugenzi na madiwani ni kuhakikisha fedha zinazokuja kwa ajili ya mikopo ya vikundi vya Wanawake na Vijana kuhakikisha zinawafikia ili kuwawezesha kuendeleza shughuli zao za ujasilimali na kupata kipato.


Mariamu alisema kwa sasa hawatakubali kuona fedha zinakuja kwa ajili ya mikopo ya Wanawake na Vijana kisha zinapelekwa kwenye shughuli nyingine na kuwaacha Wanawake na Vijana wakiendelea kukosa fedha hizo na kuendelea kuwa masikini.


Awali Afisa Mtendaji wa Kata ya Mukendo Roda Laurian alisema ana amini Wanawke hao hawatashindwa kurejesha fedha hizo kwa kuwa zinalejeshwa baada ya miezi sita kwa asilimia tano na kuwataka Wanawake hao kuhakikisha fedha hizo wanazitumia kwa malengo yaliyokusudiwa.

Post a Comment