0














MBUNGE wa jimbo la Musoma mjini Vicent Nyerere amesema kuwa idara nyeti za serikali mkoani Mara ndizo zinazoongoza kwa kudaiwa deni kubwa la maji ikiwemo ikulu ndogo.

Mbunge huyo aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akiwahutubia maelfu ya wananchi wa mji wa Musoama na vitongoji vyake katika mkutano wake wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule sekondari Mara.

Nyerere alisema kuwa ofisi ya mkuu wa mkoa yaani nyumbani kwa mkuu wa mkoa inadaiwa shilingi 10,592,668.70, Magereza  mkoa wanadaiwa shilingi 1,275,585.97,mganga mkuu wa mkoa anadaiwa shilingi 35,352,117,50,wakala wa barabara mkoa wanadaiwa shilingi 920,373,00.

Alizitaja idara nyingine zinazodaiwa deni hilo kubwa kuwa ni pamoja na  JWTZ  Makoko wanaodaiwa shilingi   1,180,466.00,shirika la umeme Tanesco wanadaiwa shilingi 2,193,027,55  ,ofisi ya kamanda wa polisi Mara wakidaiwa shilingi 91.361,438.00

Alisema kuwa kama pesa hizo zingekuwa zimelipwa kwa mamlaka ya maji Musoma ,Muwasa ingeweza kujiendesha  ambapo alisema anashangazwa na wasimamizi wa idara hizo kwa kulipa madeni hayo wakati serikali ikituma pesa nyingi.

‘’Nataka niwaambie nakwenda bungeni nitapeleka hoja binafsi ya kutaka kufahamu ni kwa nini idara hizo hazilipi bili ya maji kwa Muwasa maana hii ni kuzidi kudhoofisha idara hiyo’’alisema mbunge huyo.

Alisema kuwa kama pesa hizo zingekuwa zimelipwa kwa Mamlaka ya Maji Musoma (Muwasa) ingeweza kujiendesha  ambapo  alishangazwa na wasimamizi wa idara hizo kwa kutolipa madeni hayo wakati Serikali ikituma pesa nyingi.

Kwa upande wake meya wa manispaa ya Musoma Alex Kisurura alisema kuwa wananchi wa Musoma wanachohitaji ni maendeleo na wala si porojo za akina Nape na Kinana hivyo wananchi watafakali wenyewe na kuona mahali ukweli ulipo.

Meya  huyo aliwaambia wananchi hao kuwa Chama hicho kitaendelea kuwatumikia Wananchi kwa maana walikiamini na wakakichagua hivyo hakitawaangusha bali waendelee kukiamini.

‘’Nawaambieni leo nimesaini mikataba mitatu ofisini kwangu ya matengenezo ya barabara katika maeneo mbalimbali ya Nyakato,Kwangwa,Nyamatare na hivyo wananchi msihofu achaneni na uongo wa Nape CCM sasa haina sera kila kukicha ni kuisema chadema tu hawazungumzi namana ya kukinusuru chama chao’’alisema Kisurura.




Post a Comment