0

TAASISI ya Kuzui na Kupambana na Rushwa mkoani Mara imemfikisha Mahakamani Mwalimu Shija Lutonja wa Shule ya Msingi Baruti iliyopo Manispaa ya Musoma kwa kosa la kutumia hati ya ndoa pamoja na cheti cha kuzaliwa cha mtoto vyote vikiwa vya kughushi na kujipatia fedha zisizo halali kiasi cha shilingi milioni moja laki nne na sitini na tano elfu kutoka kwa mwajili wake Halimashauri ya Manispaa ya Musoma.  

Kujipatia kiasi hicho cha fedha kwa mwalimu huyo ni kinyume na Kifungu cha 22 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007 pamoja na aya ya 10(1)kifungu cha 57(1) cha Jedwali la kwanza la Sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 200.

Mbele ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Musoma Joyce Mkhoi,ilidaiwa na mwendesha mashitaka wa Takukuru Kheri Mchome ilidaiwa mnamo mwezi machi mwaka huu mwalimu huyo  aliwasilisha hati ya ndoa ikionyesha ikionyesha alifunga ndoa na Ester Francis na ana mtoto aitwaye Shija Lutonja na kulipwa kiasi cha shilingi 1,465,000 kama fedha zaa kujikimu na mtoto huyo bandia.

Ilidaiwa na mwendesha mashitaka huyo kitendo cha kughushi vyeti hivyo na kujipatia kiasi hicho cha fedha kimeisababishia Manispaa ya Musoma na Serikali hasara ya kiasi cha shilingi 1,465,000/=kinyume na aya ya 10 kifungu cha 57(1) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 200 na hivyo kumfungulia kesi ya jinai namba 5 ya mwaka 2013.

Mshitakiwa huyo amekana mashitaka yake na kupelekwa rumande baadaa ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana hadi kesi hiyo itakapotajwa tena tarehe 2 octoba mwaka huu.

Baada ya kusikiliwa kesi hiyo,Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mara Holle Makungu alizungumza na blog hii na kuwaasa walimu pamoja na watumishi wa umma kwa ujumla kujiepusha na ndoa za kughushi ili kuwawezesha kulipwa fedha nyingi kwani madhara yake ni makubwa pale inapotokea mtumishi huyo amefariki kabla ya kustafu.

Alisema kitendo hicho lichja ya kwamba ni kinyume na makosa pia itawapa tabu wasimamizi wa mirathi na warithi halali wa marehemu kupata shida kubwa kupata mafao kutoka mifuko ya hifadhi ya jamii kutokana nakumbukumbu zao kuonyesha watu wasio stahili wanaopaswa kupata mgawo wa mafao yatokanayo na marehemu.

Makungu alisema ni vyema kufuata taratibu zote za utumishi zinavyoelekeza na si vyema kutaka malipo makubwa ya haraka haraka bila kufuata taratibu kitendo ambacho si sahihi kwa mujibu wa maadili ya kazi za utumishi wa umma na kuongeza kuwa kama mtu anataka kuoa ama kuolewa nivyema akafuata taratibu.

Mkuu huyo wa Takukuru,alisema maafisa wa taasisi hiyo wataendelea na majukumu yao ya kufatilia vitendo vyote vinavyofanywa na watumishi wa umma wasi waaminifu vya kuvunja maadili ya utumishi kisha kuwafikisha katika vyombo vya sheria na kuwataka watumishi kutokwenda kinyume na taratibu.

Post a Comment