0


WAKULIMA  wa  zao la Mpunga katika mradi  wa Umwagiliaji wa Irienyi wilayani  Rorya mkoani Mara,wamemuomba  Waziri Mkuu Mizengo Peter Pinda kufutilia utekelezaji wa ahadi  yake  ya kuwapatia  trekta tatu ndogo  za kulimia (Powertiller) ambayo alitoa   miaka miwili  iliyopita baada ya kujionea  kilimo hicho.
 
Walisema ingawa Waziri Mkuu alitoa ahadi ya kutoa powertiller mbili pia  alimuomba mbunge wa jimbo la Rorya Lameck Airo kumuunga mkono kwa  kununua kwa kununua moja lakini hadi sasa wameweza kukabidhiwa mbili moja wapo ikiwa ni mbovu.
 
Akizungumza na Rai  mwakilishi wa  skimu ya umwagiliaji  wa kilimo cha mpunga Irienyi ,amesema  tangu  waziri mkuu atoe  ahadi hiyo  ili kuwasaidia kubadili  kilimo hicho kutoka katika jembe la mkono  wameweza kupokea powertiller  mbili  ndogo  moja ikiaribika kwa muda mfupi huku moja ikishindwa  kuwasilishwa katika kutekeleza ahadi ya waziri mkuu na mbunge huyo.
 
“Tuliona  wemeleta powertiller mbili, moja  ilikuwa kama imetumika  sasa hatujui  ni  ya  waziri  mkuu  au mbunge,tumekuwa gizani kila  tukiohoji  kupata ya tatu kama ahadi ilivyokuwa  wakati  mwingine  tunatishwa na viongozi wetu  wa  kijiji  kuwa  ahadi  ya  waziri  mkuu haipaswi kuhojiwa”alisema  mwakilishi  huyo  wa  wakulima hao aliyeomba kutotajwa jina gazetini.
 
Alisema  vitisho hivyo  vimewaweka katika mashaka kuwa  inawezekana waziri  mkuu  tayari  alishatoa  fedha  kwaajili  ya kununuliwa  zana hizo   mpya lakini baadhi  ya  wajanja  wamezitumia  na kutuletea  moja ya powertiller  hizi mbili moja ikiwa ni mbovu.
 
“Kweli inawezekanaje waziri mkuu atoe  ahadi ya kununua power tiller kisha moja akachukue  yake  shambani atuletee,hali hii inatutia mashaka ndio maana tunaambiwa hakuna kuhoji,eti tukihoji tu tunaweza kukamatwa au  akija mgeni mwingini hauteletwa hapa kwetu”aliongeza.
 
Hata hivyo katibu mpya wa Skimu hiyo ya umwagiliaji,alipoulizwa kwa njia ya simu,alisema wakati powertiller hizo zikipokelewa alikuwa si kiongozi kwa wakati huo lakini alipata taarifa kuwa zana hizo ni ahadi ya Waziri Mkuu na moja iliyobaki inawezekana ikawa ya mbunge ambaye almuunga mkono waziri mkuu katika kuwasaidia wakulima hao.
 
“Nilipochaguliwa  niliambiwa hizi mbili ni ahadi ya waziri mkuu,lakini moja ilifanya kazi kwa muda mfupi tu sasa sijui ililetwa ikiwa na ubovu ila hadi  sasa hatujapata ile  ya tatu, sisi tulichukulia  zote  zilitokana na kauli  ya  waziri mkuu, lakini sasa tunaambiwa  mbunge ndiye alitoa ahadi  ya uongo  kwa waziri mkuu kwa hiyo pikipiki ya tatu”alisema Mwita.
 
Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Rorya Lameck Airo,alipoulizwa kuhusu kushindwa kutekeleza  ahadi hiyo  ambayo  aliitoa  kwa kumuunga  waziri mkuu,alikanusha vikali na kusema tayari alitoa kiasi cha shilingi milioni 8.8  kwa ofisi ya mkuu wa mkoa kwaajili ya kununulia  power tiller hiyo.
 
“Kweli nilitoa  ahadi hiyo kwaajili ya kumuunga mkono Waziri Mkuu ili aweze kutoa powertiller tatu moja ikiwa ni yangu, lakini siku tulipokuwa kwenye  kikao cha majumuisho  pale mkoani  nilitoa  fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni 8.8  kununulia trekta hiyo  ndogo  zilokuwa zimeletwa na watu  wa  SUMA JKT pale nje kwa RC (mkuu wa mkoa) sasa iweje hadi leo hawajapata au wamepelekewa mbovu?alihoji na kuongeza.
 
“Nillipotoa fedha hizo  tulionyeshwa  zile  powertiller  nilienda nikaiwasha ilikuwa  nzima tena mpya iweje leo wananchi wapelekewe mbovu?mimi nadhani fuatilia kwa mkuu wa mkoa wa ndo watajua iko wapi hiyo”aliongeza Airo.
Aliongeza kuwa kwa  vile tayari alitoa  fedha  tena kwa kuzikabidhi kwa mamlaka za serikali hivyo anatambua kuwa powertiller yake ndiyo iliyokabidhiwa kwa  kikundi hicho hivyo ni jukumu  la  uongozi wa mkoa kufuatia fedha hizo na kununua powertiller mpya na kuikabidhi  kwa wakulima  wa Skimu hiyo ya Irienyi  ili  kutekeleza  ahadi ya Waziri Mkuu.
 
Mkuu wa mkoa wa Mara aliikuta ahadi hiyo  John Tuppa,alipoulizwa kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kuhusu  utata wa ahadi hiyo  ya waziri mkuu,ameahidi  kufuatilia suala hilo.

Post a Comment