WAZABUNI wa mkoani Mara wameoneshwa kusikitishwa kwa kile walichodai mkakati wa Serikali unaolenga kuwafilisi kwa kushindwa kulipa kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 2.5 zinazotokana na madai mbalimbali huduma zilizotolewa katika katika taasisi mbalimbali za Serikali mkoani humo.
Kiasi hicho
cha fedha kinadaiwa na Wazabuni hao wa mkoa wa Mara baada ya kutoa huduma mbalimbali vikiwemo vyakula na mahitaji mengine muhimu katika vyuo
vya ualimu,vyuo vya afya,Shule za Sekondari na Magereza.
Mwenyekiti
wa wazabuni wa mkoa wa Mara Edward Mohere,aliwaambia waandishi wa habari mjini
Musoma, kuwa kushindwa kwa Serikali kuwalipa wazabuni hao wa ndani ni mkakati maalum wa kuwafilisi hatua ambayo pia itachangia kuwaumiza
wakulima ambao wamekuwa wakiuza mazao yao kwa mkopo.
Alisema
wanasikitishwa na kauli za mara kwa mara za Serikali ya kuwalinda wafanyabiashara wa ndani katika kuhakikisha wanachangia kuinua
uchumi na kutoa ajira kwa vijana lakini badala yake imekuwa ikikopa
bidhaa,vyakula na mahitaji mengine kutoka kwa wafanyabiashara hao bila kulipa
kwa kipindi kirefu sasa.
“Tulifikiria
tuishitaki Serikali lakini tukasema tunaamini
chini ya Rais Jakaya Kikwete tutangulize
mbele uzalendo na kwamba serikali italipa deni letu hili nasi tulipe wanaotudai
tena kwa riba wakiwemo wakulima lakini hadi sasa zimekuwa chenga”alisema Mohere
na kuongeza.
“Kwa mfano
juzi kuna wenzetu wemeuziwa nyumba zao na mabenki kwa kushindwa kulipa deni kwa
wakati sasa wao na familia zao zinateseka hivi kweli hapa kuna haki kama si
mkakati maalum wa kutufilisi”alihoji.
Hata hivyo mwenyekiti
huyo wa Wazabuni mkoani Mara,alisema amefurahishwa na kauli ya Rais Kikwete
aliyoitoa mkoani Iringa kuwa ni aibu kwa serikali kudaiwa na wakulima hivyo
kutaka mamlaka za serikali kuondoa aibu hiyo ambayo sasa Serikali inaipata kwa
kudaiwa na wazabuni.
“Tumetoa
huduma bila vikwazo sasa kwanini kwenye kulipa kuwe na vikwazo?sisi hatuwezi
kutoa rushwa ili tulipwe haki yetu hivyo ni jukumu la serikali kulipa madeni
kama ilivyopata huduma kutoka kwetu”alisisitiza Mohere.
Mwishoni mwa
mwaka jana katibu mkuu wa wizara ya elimu,afya na mambo ya ndani ya nchi kwa
nyakati tofauti walikiri kudaiwa na wazabuni hao huku wakidai madeni hayo
yatalipwa katika bajeti ya mwaka huu wa fedha (2013/4) kitu ambacho kinadaiwa kutotekelezwa.
Katika kikao
chao cha mwaka jana wazabuni hao walifikia azimio la kusitisha kutoa huduma kwa
taasisi za Serikali na kutaka kuishitaki Serikali kabla ya kuonyesha uzalendo
huo kwa kusitiza uamuzi huo ili kuipa
nafasi serikali kushughulikia madai yao.
Post a Comment
0 comments