NI MICHEZO NA BURUDANI |
MKUU WA WILAYA AKIINGIA KUFUNGUA |
HAPA ANATETA NA AFISA MICHEZO MANISPAA YA MUSOMA SHEKHDADI SAIDI |
WANAMICHEZO WAKIINGIA UWANJANI TAYARI KWA KUANZA MICHEZO |
TUKIPWA NAFASI TUNAWEZA
BANGO LAJIELEZA KUTOKA MKOANI KAGERA |
MWANARIADHA MLEMAVU WA AKILI |
MWENGE WA OLYMPICS MAALUM
MBIO ZA MWENGE WA OLYMPICS |
MKUU WA WILAYA YA MUSOMA JACKSON MSOME AKIPOKEA MWENGE WA OLYMPICS MAALUM
MKUU WA WILAYA AKIZINDUA MBIO ZA MITA MIA MOJA ZA WALEMAVU WA AKILI
PICHA YA PAMOJA
TUNAWEZA
MKUU
wa Wilaya ya Musoma Jacksoni Msome amewataka wazazi na walezi
kutowaficha majumbani watoto wenye Ulemavu bali wawatoe na
wawashilikishe kwenye shughuli mbalimbali za kijamii ikiwe sekta ya
michezo ili kuwajengea utimamu wa mwili na akili.
Kauli
hiyo ilitolewa katika ufunguzi wa michezo kwa wanafunzi wenye ulemavu
wa akili(Special Olympics) iliyofanyika kwenye uwanja wa kumbukumbu ya
karume mjini hapa huku ikiwashilikisha wanamichezo 107 kutoka mikoa ya
Mwanza,Kagera pamoja na Mara.
Alisema
michezo ina umuhimu mkubwa kwa wanafunzi wanaoishi na ulemavu wa akili
ili kuweza kukuza uwezo wa kufikili,viungo kuwa na mnyumbuliko,kukuza
utimamu wa mwili na akili,kuongeza ujasili na kujiamini,kujenga
mahusiano
na kusaidia kukuza jiografia ya mtoto.
Msome
alidai Special Olympics inawajenga wenye ulemavu hususani ulemavu wa
akili na kuondoa dhana potofu iliyojengeka ndani ya jamii ya kuwatenga
na kutowapa nafasi kwa kisingizio kwamba watoto wenye ulemavu wa akili
hawawezi kumudu stadi zozote.
Mkuu
huyo wa Wilaya ya Musoma alitoa wito kwa wazazi,jamii,taasisi
mbalimbali pamoja watu binafsi kuwapa kipaumbele walemavu wa akili kwa
kuwapa nafasi ya kushiriki michezo ili iwajengee uwezo wa kumudu stadi
mbalimbali na kuwataka wadau kuunga mkon jitihada zinazofanywa katika
kuendeleza upatikanaji wa mahitaji kwa watoto wenye ulemavu wa akili.
Kwa
upande wake mwenyekiti wa kamati ya Special Olympics mkoa wa Mara
Paschal Kafubhi alisema zipo
changamoto zinazowakabili watoto wenye ulemavu wa akili ikiwa ni pamoja
na kufichwa ndani na familia,kutengwa na jamii na kusababisha wadau
mbalimbali kutoona umuhimu wa kuwasaidia na kuwaendeleza.
Alisema
kutokana na kuwa na changamoto nyingi ya kufanikisha mashindano hayo
ambayo yanafanyika kikanda kwa mara ya kwanza mkoani Mara,Mwenyekiti
huyo alilishukuru Shirika la Lilian Foundation la Uholanzi pamoja na
Shirika la Lake Victoria Disability la mjini Musoma kwa kufanikisha
kufanyika kwa mashindano hayo.
Post a Comment
0 comments