0
OFISI MPYA ZA PSPF ZILIZOPO MJINI MUSOMA




WAJASILIAMALI WAKIPEWA MAELEZO


AFISA MFAWIDHI WA PSPF MKOA WA MARA SUDI HAMZA AKIMUHUDUMIA MWANACHAMA KATIKA OFISI ZA MFUKO HUO JENGO LA TTCL MJINI MUSOMA

Afisa Mfawidhi wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) mkoa wa Mara Sudi Hamza.amewataka Wajasiliamali kuweka utaratibu wa kujiwekea akiba katika mifuko ya pensheni ili kujipatia mafao ambayo yataweza kuwakomboa kipindi ambacho mjasiliamali atakuwa amekwama katika jambo lolote.

Akizungumza na blog hii ofisini kwake,Sudi amesema mfuko wa uchangiaji wa hiari ulioanzishwa na (PSPF) lengo lake hasa ni kuwawezesha wajasiliamali kujiwekea akiba baada ya mifuko mingi kuwalenga watumishi wa umma na kada nyingine.

Amesema wajasiliamali wanapaswa kuangalia faida ya kujiwekea akiba kwani humkomboa pale atakapokwama ikiwa ni suala la ada ya elimu ama kujiongezea  mitaji katika biashara pale kutakapotokea kukwama na kuhitaji mafao ya kujikomboa.

 Amedai mwanzoni mfuko  huo ulikuwa ukiwatazama watumishi wa umma peke yao katika kujiwekea mafao ya pensheni na kusema hiyo ni fursa nyingine kwa wajasiliamali pamoja na watu wengine wasio watumishi wa umma katika kujiwekea akiba.

 Akizungumzia fao la kujitoa ambalo limekuwa likizungumziwa usumbufu wake kwa baadhi ya mifuko,Sudi amesema PSPF kitu ambacho inakizingatia ni kutomuona mwanachama wa mfuko huo akiangaika katika kufatilia mafao.

Amesema utaratibu uliopo wa mwanachama kuandika barua mapema juu ya kutaka kujitoa ama kuhitaji mafao kwa ajili ya elimu ama ujasilimali unasaidia kumuandalia mwanachama fao lake kwa muda anaohitaji bila kumletea usumbufu.

Afisa huyo wa PSPF amesema kwa muda wa siku tatu tangu waanze uhamasishaji wa uchangiaji wa hiari jumla ya wanachama 26 wameshajiungwa nakuwaomba wajasiliamali wa mkoa wa mara kufika katika ofisi mpya za mfuko huo zilizopo katika jengo la shirika la simu TTCL mjini musoma waweze kujiunga

Post a Comment