WANAFUNZI WAKIWA NJE YA DARASA
WIMBO WA TAIFA KABLA YA KUANZA BARAZA
MWANASHERIA WA MANISPAA YA MUSOMA AKITOA UFAFANUZI
MKURUGENZI WA MANISPAA YA MUSOMA AKITOA UFAFANUZI KWENYE BARAZA
DIWANI WA KATA YA MAKOKO ALOYCE MAWAZO AKISISITIZA HATUA KUCHUKULIWA
DIWANI WA KATA YA MWISENGE ANGELA DERRICK ALIYESIMAMA KATIKATI NI DIWANI OCHALO ALIYETUHUMIWA
 
WIMBO WA TAIFA KABLA YA KUANZA BARAZA
MWANASHERIA WA MANISPAA YA MUSOMA AKITOA UFAFANUZI
MKURUGENZI WA MANISPAA YA MUSOMA AKITOA UFAFANUZI KWENYE BARAZA
DIWANI WA KATA YA MAKOKO ALOYCE MAWAZO AKISISITIZA HATUA KUCHUKULIWA
DIWANI WA KATA YA MWISENGE ANGELA DERRICK ALIYESIMAMA KATIKATI NI DIWANI OCHALO ALIYETUHUMIWA
IMEAMULIWA
 kufunguliwa taarifa polisi "RB" na Baraza la Halimashauri ya Manispaa 
ya Musoma juu ya uhalibifu wa majengo sita ya madarasa unaodaiwa 
kufanywa na Diwani wa Kata ya Kigera Gabriel Ochalo(CUF) pamoja na 
Kamati ya shule ya msingi Kigera A kuanza muhula wa masomo 2014.
Naibu
 Meya wa Halimashauri hiyo Bwire Nyamwero ambaye pia ni Diwani wa Kata 
ya Mwisenge(CHADEMA) alifikia maamuzi hayo baada ya Diwani wa Kata ya 
Bweri Zedi Sondobhi (Chadema) kuomba Baraza lililokuwa na kikao cha 
kujadili na kupokea rasimu ya bajeti ya mwaka 2014-2015 kuzungumzia 
suala la uharibifu wa madarasa uliofanywa katika shule hiyo.
Sondobhi
 alisema katika muhula huu wa masomo wanafunzi wa shule ya msingi Kigera
 A wameshindwa kuhudhulia vipindi madarasa kwa kile kilichoonekana 
majengo sita ya shule hiyo kung'olewa mabati na kushindwa kuezekwa hali 
inayofanya wanafunzi kushindwa kusoma na kuwaaomba madiwani wakubali 
hoja yake na kujadili hali hiyo.
Katika
 majadiliano kuhusiana na hali hiyo,Mkurugenzi wa Halimashauri ya 
Manispaa ya Musoma Ahmed Sawa hakuwa na barua yoyote wala maagizo ya 
kuondolewa mabati ya shule hiyo hali iliyomfanya Naibu Meya kuomba 
maelezo ya kina kutoka kwa Diwani wa Kata husika juu ya uhalibifu 
uliofanywa kwenye shule hiyo.
Akizungumzia
 hali hiyo,Diwani wa Kata ya Kigera Gabriel Ochalo alilieleza Baraza 
hilo kusika kuwepo kwenye kikao cha Kamati ya shule kilichoamua kuondoa 
mabati ya majengo sita ya madarasa pamoja na kupaua kuta za majengo hayo
 baada ya kupokea kiasi cha shilingi milioni 3 na laki 5 kwa ajili ya 
ukarabati wa shule hiyo.
"Ni
 kweli nilikuwepo kwenye kikao hicho cha kamati
 ya shule kama mjumbe na baada ya kuona fedha
 hizo zimekuja na kutokana na uchakavu wa madarasa tuliamua kufanyia 
ukarabati lakini baada ya kuezua darasa moja yote yalitikisika na kuamua
 kuondoa madarasa yote na ndio maana hadi sasa kuna kukwama 
kunakoonekana,"alisema Ochalo.
Kufuatia
 majibu hayo mjadala mzito uliibuka kutoka kwa madiwani baada ya kudaiwa
 Diwani huyo akuzingatia taratibu na kushiriki katika shughuli ambayo 
imepelekea kushindwa kwa wanafunzi
 kuhudhuria vipindi madarasani na
 kuomba hatua zaidi zichukuliwe kwa wale wote waliohusika na uvunjwaji 
wa madarasa hayo.
Diwani
 wa Kata ya Makoko Aloyce Mawazo(CHADEMA) alisema hakuna sababu ya 
kuoneana aibu wala huruma kuhusiana na suala hilo kwa kuwa wanaoathirika
 ni wanafunzi na wazazi hivyo Diwani na wote waliohusika lazima 
wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria na madarasa hayo yaezekwe mara 
moja ili wanafunzi waendelee na masomo.
Kutokana
 na mjadala huo ulichukua zaidi ya masaa mawili Naibu Meya alimuamulu 
Afisa Elimu Msingi kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa juu ya 
uharibifu huo ili vyombo vya sheria viweze kuchukua hatua huku kamati ya
 maadili nayo ikitarajiwa kulizumzia suala hilo katika vikao vyake.
Kwa
 upande wake Afisa Elimu Msingi Daniel Makorere mara baada ya kutoka 
kituo cha polisi Musoma kati alizungumza na Waandishi wa Habari na kudai
 kuwa tayari ameshatoa taarifa polisi juu ya uharibifu huo na 
kufunguliwa taarifa ya uharibifu wa mali ya umma yenye namba 
MUS/RB/480/2014.
Alisema
 ofisi yake ilipeleka kiasi cha shilingi milioni 3 n laki 5 kwa ajili ya
 ukarabati wa jengo moja la darasa lakini kubomolewa kwa majengo sita 
hana taarifa zozote na amepokea maagizo ya Baraza hilo na kutoa taarifa 
polisi juu ya Diwani huyo.
Katika
 kikao hicho
 madiwa walipitisha bajeti ya shilingi bilioni 30 ikiwa ni ongezeko la 
asilimia 38.73 ya shilingi bilioni 21 zilizopitishwa kipindi cha mwaka 
wa fedha 2013-2014 ikiwa ni ongezeko katika mradi wa kuboresha barabara 
na ongezeko la mishahara kwa watumishi wapya wa Halimashauri ya Manispaa
 waliopata ajira mpya kwa mwaka wa fedha 2014-2015













Post a Comment
0 comments