0

MKURUGENZI WA HALIMASHAURI AKITOA TAARIFA
MWENYEKITI WA HALIMASHAURI KULIA AKISIKILIZA KWA MAKINI
BARAZA
MKRUGENZI WA HALIMASHAURI AKIFAFANUA JAMBO
DIWANI AKITAFAKARI JAMBO BAADA YA KUCHANGIA!
MADIWANI SERENGETI KWENYE KIKAO CHA BAJETI
KUWEKA KUMBUKUMBU SAWA
HALIMASHAURI ya Wilaya ya Serengeti imepanga kufikia sifuri tatu katika mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi kwa kutoa elimu ya kutosha ambayo itamfikia kila mwananchi kuhusiana na athari za ugonjwa huo.

Katika taarifa yake kwenye kikao cha Baraza la madiwani cha kupokea,kujadili na kupitisha mapendekezo ya mpango wa bajeti ya mwaka 2014-2015,Mratibu wa Mpango wa Kudhibiti Ukimwi Wilaya ya Serengeti Elly Msamisa alisema wamepanga kutoa elimu kwa njia mbalimbali ili kufikia mipango hiyo.

Alisema elimu kuhusiana na masuala ya Ukimwi kwa jamii itatolewa kupitia sinema,vikundi vya uelimishaji,kusimamia kwa karibu Kamati za Kudhibiti Ukimwi ngazi ya Kata na Vijiji pamoja na kushirikiana na wadau wa mapambano dhidi ya Ukimwi wilayani Serengeti.

Msamisa alisema matarajio ni kufikia sifuri tatu ambazo ni maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi sifuri,vifi vitokanavyo na ukimwi sifuri pamoja na ubaguzi na unyanyapaa wa waathirika wa ukimwi kufikia asilimia sifuri.

Alisema kitengo cha kudhibiti ukimwi wilayani kimepanga kuimalisha mwitikio wa jamii katika mapambano dhidi ya ukimwi,kupunguza hatari ya maambukizi mapya katika sehemu hatarishi pamoja na kuimalisha uwezo wa kiuchumi kwa makundi yanayoishi na virusi vya ukimwi na ukimwi.

Alidai katika kipindi cha bajeti ya mwaka 2012-2013 kulikuwepo na  changamoto mbalimbali juu ya utekelezaji wa shughuli za mapambano dhidi ya ukimwi kwenye kitengo cha kuratibu shughuli za ukimwi na kufanya kazi kutokufanyika kwa usahihi.

Mratibu huyo wa Ukimwi Wilaya ya Serengeti alisema baadhi ya changamoto hizo ni ni idara za Halimashauri kutokuweka katika bajeti zao masuala ya ukimwi na hata za kusaidia watumishi wanaoishi na virusi vya ukimwi katika idara zao.

Akichangia taarifa hiyo,Diwani wa Kata ya Manchila Michael Shaweshi alisema ili Wilaya ya Serengeti itoke kwenye asilimia 4 ya maambukizi kimkoa inapaswa kila Diwani kuwa na mipango ya kupambana na ukimwi wilayani Serengeti.

Madiwani wa Halimashauri hiyo kwa pamoja walipitisha bajeti ya mwaka 2014-2015 kiasi cha shilingi  bilioni 31 ikiwa ni ongezeko kutoka bilioni 23 zilizopitishwa katika kipindi cha mwaka 2012-2013 ambazo zitafanya kazi mbalimbali za kimaendeleo na miradi ikiwemo mapambano dhidi ya ukimwi

Post a Comment