0


Arsenal imepata pigo baada ya mchezaji wake Theo Walcott kuthibitishwa kuwa atakosa kushiriki michuano ya Kombe la dunia kwa kuwa atakuwa kando kwa takriban miezi sita baada ya kupata jeraha la mguu. 

mshambuliaji huyu wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24 alipata jeraha wakati wa michuano ya Kombe la FA siku ya jumamosi walipokutana na Tottenham na kuichapa mabao 2-0.
Taarifa ya klabu ya Arsenal imesema Walcott atafanyiwa upasuaji siku zijazo na atakua nje ya dimba kwa takriban miezi sita ambapo atakosa mechi zote zilizobaki za msimu huu sambamba na Kombe la dunia.

Michuano ya Kombe la dunia inatarajiwa kuanza tarehe 12 mwezi Juni, huku Uingereza ikitarajiwa kukipiga na Italia katika mchezo wake wa kwanza siku mbili baadae.

Rekodi ya Walcott akiwa na Kikosi cha Uingereza.

-Alionekana kwa mara ya kwanza na kikosi cha Uingereza mwaka 2006 ilipocheza na Hungary.

-Alisisimua wengi baada ya kuwa katika kikosi hicho kwenye Kombe la dunia mwaka 2006 akiwa na umri wa miaka 17 kabla ya kuingia kwenye ligi kuu nchini Uingereza.

-Aliwahi kufunga mabao matatu dhidi ya Croatia mwezi Septemba mwaka 2008.

-Katika hatua ya kushangaza aliachwa katika kikosi kilichocheza michuano ya kombe la dunia mwaka 2010 nchini Afrika kusini.

Walcott alichukuliwa kutoka Southampton mwaka 2006 kwa kititta cha Pauni milioni 12.5.

Post a Comment