0
                                                            


Watuhumiwa wa usafirishaji wa Meno ya Tembo ambao wamekamatwa wilayani Nanyumbu Mkoa wa Mtwara wakiwa wanaangalia upimaji uzito wa meno hayo yenye uzito  wa kg 130.6 yenye thamani ya Tshs Milioni 7.35 katika ghala lililopo makao makuu ya wilaya hiyo mjini Mangaka kutoka kulia ni Hamidu Ngunde (40) wa pili ni Boniphace Msogo (29) na Geddat Mmuni (36) ote wakazi wa Jijini Dar es Salaam. (Picha na Thomas Dominick)




Mkuu wa Kituo cha Polisi Mangaka Makao makuu ya Wilaya ya Nanyumbu Alfred Mbena akiwa na askari wengine wakiangalia meno ya  tembo 58 yenye uzito wa Kg 130.6 yenye thamani ya Tshs Milioni 7.35 ambayo wameyakamata katika kijiji cha Chungu  tayari kwa kusafirishwa kwenda Jijini Dar es Salaam. (Picha na Thomas Dominick)

 
Mama Nyama wa Wilaya ya Nanyumbu  Consolata Mmuni akiangalia upimaji wa meno ya tembo ambayo yamekamatwa katika kijiji cha Chungu Meno hayo yenye uzito  wa Kg 130.6 Yenye thamani ya Tshs Milioni 7.35. (Picha na Thomas Dominick)




Watuhumiwa wa usafirishaji wa Meno ya Tembo ambao wamekamatwa wilayani Nanyumbu Mkoa wa Mtwara  yenye uzito  wa kg 130.6 yenye thamani ya Tshs Milioni 7.35 katika  Hamidu Ngunde (40) wa pili ni Boniphace Msogo (29) na Geddat Mmuni (36) ote wakazi wa Jijini Dar es Salaam wakiwa ndani ya gari la polisi baada ya kumaliza upimaji wa uzito . (Picha na Thomas Dominick
 Konstabo Magreth wa Kituo cha Polisi Mangaka wilaya ya Nanyumbu akiwa anaangalia meno ya Tembo ambayo yamewekwa chini baada ya kukamatwa kijiji cha Chungu wakiwa tayari kusafirishwa kwenda Jijini Dar es Salaam
 Wananchi wakichungulia ndani ya ghala la kijiji cha Mangaka wakati askari jeshi la polisi(hawapo pichani) wakipima meno ya tembo ambayo wameyakamata

Mkuu wa Kituo cha Polisi Mangaka Makao makuu ya Wilaya ya Nanyumbu Alfred Mbena akiwa ameshik moja ya meno ya tembo na askari wengine wakiangalia meno ya tembo 58 yenye uzito wa Kg 130.6 yenye thamani ya Tshs Milioni 7.35 ambayo wameyakamata katika kijiji cha Chungu tayari kwa kusafirishwa kwenda Jijini Dar es Salaam. (Picha na ThomasDominick)  
 
 
 Meno ya tembo yakiwa chini baada ya kupimwa katik ghala la kijiji cha Mangaka

Hili ndilo gari aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili T 208 AGC mali ya Hilary Hemed Rashid ambalo lilikuwa linatumika katika usafirishaji wa meno ya tembo.




 
Na Thomas Dominick,
Nanyumbu

JESHI la Polisi Mkoa wa Mtwara limefanikiwa kukamata nyara za Serikali ikiwa ni meno ya tembo 58 sawa na tembo 29 yenye uzito wa kilogramu 130.6 yenye thamani ya Tshs Milioni 7.35 pamoja na watuhumiwa watatu ambao walikuwa wanayasafirisha kutoka wilayani Nanyumbu kwenda Dar es Salaam.

Kukamatwa kwa watuhumiwa hao na meno  hayo ya tembo ni utekelezaji kwa viteno kwa Mkuu wa Wilaya hiyo Festo Kiswaga maelezo na maagizo ya Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete vita dhidi ya ujangiri.

Ambapo inadaiwa kuwa baada ya kukamatwa watuhumiwa hao walishuka kwenye gari na kukiri kuwa wamechukua meno ya tembo na kuyasafirisha jijini Dar es Salaam na kuwaomba wayazungumze ambapo walikuwa tayari kutoa Tshs Milioni 15 kwa polisi waliowakamata.

Tukio hilo ambalo limetokea Februari 14 mwaka huu saa 11 alfajiri ambapo polisi wa wilaya ya Nanyumbu walipata taarifa kutoka kwa raia mwema ambaye aliwajulisha kuwa kuna gari linapakia meno hayo tayari kwa kuyasafirisha.
 
Watuhumiwa waliokamatwa ni Geddat Mmuni (36) dereva wa gari hilo Mkazi wa Kongowe Dar es Salaam, Hamidu Ngunde (40) Mkazi wa Mtoni kwa Aziz Ally Dar es Salaam na Boniphace Msogo (29) Mkazi wa Kimara Korogo Dar es Salaam.  

Baada ya taarifa hiyo walikwenda hadi kijiji cha Chungu na kuweka mtego kasha kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa na gari aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili T 208 AGC mali ya Hilary Hemed Rashid.

Habari za uhakika kutoka kwa mmoja wa watuhumiwa hao zilidai kuwa mmiliki wa gari ambalo limekamatwa na meno hayo ni mfanyabiashara wa biashara ya meno ya tembo kwa muda mrefu.

Mwandishi wa gazeti hili alifika katika kituo kikubwa cha polisi wilayani Mjini Mangaka na kushuhudia meno hayo ya tembo na watuhumiwa hao ambao walikuwa hawana wasiwasi wowote wa tukio hilo.

Mkuu wa upelelezi wa Wilaya hiyo Edwin John alisema kuwa baada ya kupata taarifa hiyo na kuweka mtego watuhumiwa hao waliwakama na kuwafikisha kituo cha polisi na kulifanyia ukaguzi gari.

Alisema kuwa baada ya ukaguzi huo kila sehemu na kuwabana watuhumiwa hao walionyesha sehemu ambayo walikuwa wamezihifadhi chini ya siti za kati ya gari hilo ambapo walikata na kupata uwazi wa kutosha wa kutunza.

“Kwa kweli huwezi kugundua kwa urahisi kama huna taarifa za kutosha kutoka kwa raia wema ambao wana utii wa nchi yao na hata utunzaji wao na usafirishaji wao ni mbinu mpya usiyoweza kuitambua kwa haraka,”alisema John.

Askari ambao walifanikisha kukamatwa kwa meno hayo ni D 5496 D/Sgt Mwishehe, E 5961 E/Cpl Msafiri, E 8705 D/Cpl Ng’alila (Dudu), F 4211 D/C Benson, F 6512 D/C Lugaila, F 9012 D/C Deus na G 7290 D/C Jasel wote askari wa wilaya hiyo. 

Mwandishi wa habari aliwasiliana kwa njia ya simu Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Maisha Maganga ambapo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa uchunguzi unaendelea ili kuwabaini wahusika na mmiliki wa meno.

“Taratibu zikikamilika na kuwapata wamiliki wa meno hayo ya tembo tutawafikisha mahakamani ili kujibu tuhuma za kukutwa na nyara za serikali,”alisema Maganga.

Kamanda Maganga amesema kuwa kufanikiwa kukamatwa kwa nyara hizo za serikali Jeshi hilo linajipanga kufanya doria katika barabara kuu zinazotoka na kuingia katika mkoa huo ili kukamata wahusika wa biashara haramu ikiwepo na usafirishaji wa meno ya tembo.

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo, Festo Kiswaga ambaye naye ana taaluma ya wanyama pori amewaonya wafanyabiashara wa meno ya tembo kuwa kuingia ndani ya wilaya hiyo ni rahisi ila kutoka itakuwa ngumu kwao na kuendelea kuwakamata ili kuhakikisha biashara hiyo haifanyiki ndani ya wilaya yake

“Nawatahadhaisha kuwa tupo macho kwa sasa ili kuweza kumuunga mkono Rais wetu Jakaya Kikwete katika vita ya ujangiri na uuaji wa tembo na wafanyabiashara wa meno ya tembo ambao kwa sasa wanaanza kupotea kutokana na wimbi la mauaji ya wanyama hao,”alisema Kiswaga.

Meno hayo ya tembo hadi sasa hayajulikana kama tembo hao waliuawa wilayani humo au nchi jirani ya Msumbiji ambapo tembo hao huwa wanabadilisha makazi katika nchi hizo mbili.

Tukio hilo limetokea baada ya takribani kwa miezi minne baada ya kusimamishwa kwa oparesheni tokomeza ujangiri  awamu ya kwanza ambayo ilikusudiwa kukamata majangiri ambao wanahusika na uuaji wa tembo.

Ambapo katika wilaya hiyo walifanikiwa kushika baadhi ya silaha  na watuhumiwa waliojihusisha na ujangiri zilizokuwa zinatumika katika ujangiri na nyama nguruwe tu.

Katika Oparesheni hiyo baadhi ya mawaziri walikosa nyadhifa zao baada ya wabunge kuwataka wajiuzulu kutokana askari walioshiriki oparesheni hiyo kufanya vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu.

 

Post a Comment