1
DIWANI HAILE NYUMA MWENYE SUTI NYUMA AKITOKA MAHAKAMANI

 ASKARI MAHAKAMANI

DIWANI wa Kata ya Kitaji Manispaa ya Musoma Haile Tarai (Chadema) pamoja na watu wengine watatu wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa wakidaiwa kumfanyia fujo Mjumbe wa Halimashauri Kuu ya CCM(NEC) Vedastus Mathayo katika msiba wa Shekh wa mkoa wa Mara Athumani Magee.
 

Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Faisal Kahamba,imedaiwa na mwendesha mashitaka wa polisi Jonas Kaijage mnamo January 30 mwaka huu watu hao walimsababishia usumbufu na fujo ambazo zingeweza kuhatarisha amani miongoni mwa jamii wakati Mathayo akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha mwenyewe kuelekea kuhani msiba.

Washitakiwa hao walidaiwa kutenda kosa hilo kinyume na kanuni ya adhabu kifungu cha 171(a) sura ya 16  ya mwaka 2002 na kufunguliwa kesi namba 31 ya mwaka 2014

Post a Comment

Sijaelewa habari yako ni ya kimtaa au kwa kuzingatia taaluma?kahabari yaani kapokapo tu hakana ata suluhisho,kimsingi sijakuelewa post upyaaaaaaa