0
 
 
NA ZAMARADI KAWAWA MAELEZO, DODOMA
 
Kamati ya Maridhiano ya Bunge Maalum la KATIBA waridhia Jaji Joseph Warioba kuwasilisha bungeni Rasimu ya KATIBA kwa masaa 4 Jumanne, Machi 18, 2014


Wabunge aw Bunge Maalum la Katiba wametakiwa kuhudhuria kikao cha bunge Hilo leo Jumanne Saa Tatu asubuhi hii kwa shughuli za kuapishwa kwa wabunge 30 na kumsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba akiwasilisha rasimu ya KATIBA kwa muda wa masaa 4.

Akizungumza na waandishi wa habari Mara baada ya kikao cha maridhiano kilichohudhuriwa NA takriban viongozi aw vyama vya upinzani vya CUF, Chadema, NCCR NA wajumbe wengine kilichomalizika takriban saa 3.30 usiku, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samuel Sitta amesema Jumatano kutakuwa na semina ya wabunge kuhusu kanuni za bunge Hilo.
Amesema wamekubaliana kuwa semina ya wabunge Hao kuhusu historia ya Tanzania NA Zanzibar iliyokuwa ihutubiwe NA wataalam Sita toka pande mbili za Muungano imefutwa ili kuzuia Watu wasitoe hisia zao zitakazoweza kubadili misimamo ya wabunge.
Aidha, Mheshimiwa Sita amesema kutakuwa NA semina ambapo mshauri aw Rais aw Kenya BW. Abdulkadeer NA Seneta Amos Wako watawasilisha mada kuhusu uzoefu wa Kenya katika kuandaa Katiba.
Amesema wajumbe aw Kamati ya maridhiano wamekubaliana kuwa Rais Jakaya Kikwete atalihutubia bunge Hilo Siku ya Ijumaa saa 10 jioni kwa kuwa yeye ni sehemu muhimu ya bunge Hilo.

Post a Comment