0

 
KAIMU MKUU WA TAKUKURU MKOA WA MARA ALHAJI FERUZ KORONGO
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoani Mara (TAKUKURU) imemfikisha katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime na kumfungulia kesi ya jinai namba 90 ya mwaka 2014 Mtendaji wa Kijiji cha Ryagoro wilayani Rorya Kennedy Josephat kwa kosa la kughushi sahihi za wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Kijiji hicho ili kuthibitisha uraia.

Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya ya Tarime Filbart Kilimi meidaiwa na mwendesha mashitaka wa Takukuru Kheri Mchume kinyume na kifungu cha 333,335 na 337 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.

Mwendesha mashitaka huyo wa Takukuru amedai mtendaji huyo alidanganya kwa kuandaa mukhtasari aliodai ni wa kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Kijiji ili kuonyesha kikao hicho kilikaa na kumpendekeza mtoa taarifa Takukuru(jina linahifadhiwa)ni raia wa Tanzania kwa nia ya kupatiwa cheti cha kuzaliwa huku akijua kikao hicho hakijawi kuwepo.

Amedai katika kuhalalisha udanganyifu huo mshitakiwa alighushi sahii za wajumbe 8 wa Kamati ya ulinzi na Usalama ya Kijiji kuonyesha kwamba walihudhulia kikao hicho huku akijua kuwa sio kweli bali alikuwa na lengo lake la kufanya udanganyifu na kughushi kinyume na makosa ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Mshitakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana Mahakamani hapo na kupelekwa mahabusu hadi kesi hiyo itakapofikishwa tena Mahakamani hapo kwa usikilizwaji wa awali machi 25 mwaka huu.

Wakati huo huo Kaimu Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mara Alhaji Feruz Korongo ameendelea kuwahimiza watumishi waliopewa dhamana katika shughuli za umma kutumia vizuri nafasi zao kwa kuzingatia weledi na maadili ya kazi pale wanapowahudumia watu.

Amesema kwa sasa maafisa wa Takukuru wamejipanga kuhakikisha wanazifatilia taarifa zote zinazotolewa popote pale na kuzifanyia kazi na pale yoyote atakatebainika kwenda kinyume na taratibu za kazi kwa masrahi binafsi atashughulikiwa kwa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Post a Comment