0



 KATIBU WA TIMU YA AMANI SC AKITOA MALALAMIKO KWA VYOMBO VYA HABARI
 KOCHA WA BUNDA KIDS NAYE ALILALAMIKA

 MRATIBU WA MASHINDANO YA ESTER BULAYA CUP
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Stephine Wasira pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe wametajwa na wadau wa soka wilayani Bunda kuwa ndio chanzo cha kuzuia mashindano yanayoandaliwa na Mbunge Ester Bulaya.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari kwenye uwanja wa sabasaba mjini hapa,wadau hao wa michezo wameyataja masuala ya kisiasa pamoja na viongozi hao kuwa ndio chanzo cha kupelekea kusimamishwa kwa mashindano hayo yaliyofanyika kwa miaka 4 kwa mafanikio.

Kocha wa timu ya Bunda Sports Kids Emanuel Bagoka alisema sababu zilizotolewa na chama cha soka wilayani Bunda (FAB) kutekeleza maagizo ya mkuu wa Wilaya kuhusu kuzuia mashandano hayo hazina msingi bali ni masuala ya kisiasa.

Alisema kitendo cha kutoa sababu za uwanja unaotumika mashindano hayo hauna vigezo sio ya kweli kwa kuwa uwanja huo umekuwa ukitumika kwenye mashindano mbalimbali yakiwemo ya ligi za TFF bila kuzuiliwa.

Kocha huyo alisema kitendo cha kusimamisha mashindano hayo wakati timu zimejiandaa kinaua maendeleo ya michezo na kupingana na maagizo ya Rais Kikwete kuhusu kuendelezwa kwa michezo katika ngazi mbalimbali.

Alisema Mbunge Ester Bulaya kupitia vijana(CCM) amekuwa akifanya jitihada mbalimbali za kuinua michezo katika Jimbo la Mbunda na wilaya nyingine za mkoa wa Mara lakini kinachoonekana ni kukwamishwa kutokana na masualaya kisiasa.

"Haya ni masuala ya kisiasa na viongozi wa hapa akiwemo Mbunge wa Jimbo wanahusika kutukwamisha tusiendelee na michezo...hatukubaliani na hali hii tunaomba Rais wa TFF atoe onyo kwa wanasiasa wanaoingilia michezo,"alisema mmoja wa wadau hao.

Katibu wa timu ya Amani FC James Juma alidai wamesikitishwa kwa kiasi kikubwa DC kuingilia masuala ya michezo na kutoa maagizo ya kusimamishwa na kuathiri kwa kiasi kikubwa maendeleo ya michezo.

Mwenyekiti wa Mashindano hayo Fravian Nyamageko alisema wameshangazwa na sabubu za kuzuia mashindano hayo kwa kuwa taratibu zote walizifata ya kufanyika kwa mashindano hayo ikiwa ni kufanyika kwa msimu wake wa 4.

Kwa upande wake Afisa Michezo Wilaya ya Bunda Amosi Mtani alisema hakuwa na taarifa ya kusimamishwa kwa mashindano hayo bali alipata nakala ya barua ya (FAB) ambayo pia Mtanzania inayo nakala yake ikidai wametekeleza maagizo ya DC kuzuia mashindano hayo.
 
Habari ambazo blog hii imezipata kutoka mjini Bunda zimedai kuwa baada ya wadau wa michezo kupaza sauti zao sasa mashindano hayo yameruhusiwa na kupangwa kuendelea tena hapo kesho katika uwanja wa sabasaba mjini Bunda.

Post a Comment