0


 WAZIRI MAGUFULI AKIKAGUA SEHEMU KUNAKOJENGWA DARAJA LA KYARANO KWENYE BARABARA YA MAKUTANO-NATTA-SANZANTE -MUGUMU KUELEKEA ARUSHA
 AKISHUKA DARAJA LA KYARANO
 AKIANGALIA UBORA WA UKUTA KULIA NI MENEJA WA TANRODS MKOA WA MARA EMANUEL KOROSO
 AKIPATA MAELEZO KUTOKA KWA KOROSO
 KUTOKA KUSHOTO MWENYEKITI WA BODI YA BARABARA JAMES WANYANCHA,KATI DK.MAGUFULI NA MENEJA WA TANRODS MKOA WA MARA EMANUEL KOROSO WAKIKAGUA BARABARA INAYOJENGWA NA WAKANDARASI WA NDANI
 MAGUFULI NA MKONO
 MAGUFULI AKIHUTUBIA WANANCHI WA BUTIAMA
 BAADAE WALIKWENDA KUOMBA DUA KWENYE KABURI LA BABA WA TAIFA
 VIFAA VINAVYOTENGENEZA BARABARA HIYO
WAZIRI wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuri amewataka wananchi waliovamia hifadhi ya barabara wilayani Butiama kuondoka mara moja ili kupisha shughuli za ujenzi wa barabara ya Makutano-Natta-Mugumu kuelekea Arusha.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mara baada ya kufanya ukaguzi wa ujenzi wa barabara hiyo,Waziri magufuli alisema ni vyema wale wote waliovamia hifadhi ya barabara kuondoka wenyewe kabla ya kuvunjiwa na kulipia ghalama za uvunjaji.

Alisema Serikali kwa sasa inaanda taratibu za malipo kwaajili ya fidia kwa wananchi ambao barabara inawafata kiasi cha shilingi bilioni 1.9 ambao tayari wameshapewa taarifa na wale waliovamia ni vyema wakaondoka wenyewe mapema.

“Nataka niwaambieni wananchi wa Butiama,Serikali inaendelea na jitihada za kuunganisha barabara nchi nzima lakini lazima nanyi mkubaliane na utaratibu wa kuondoka wenyewe kwenye hifadhi za barabara kabla ya kuondolewa.

“Wananchi ambao barabara inawafata hao tutawalipa fidia zao lakini wale ambao wamevamia hifadhi za barabara watakapo subiri hadi kubomolewa watagharamikia kulipa gharama za kubomoa,”alisema waziri Magufuli.

Alisema kutokana na barabara hiyo kwenda polepole wananchi wasiwalalamikie wakandarasi wanaojenga  bali kuna masuala ambayo Serikali inayashughulikia ikiwemo kuwalipa makandarasi hao zaidi ya shilingi bilioni 3 ikiwa ni malipo ya awali.

 Licha ya kudai kiasi hicho cha fedha,Waziri Magufuli amewashukuru wakandarasi hao wazalendo wenye muungano wa makampuni 10 kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo na kudai ndani ya wiki 2 watalipwa fedha zao.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo,Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Nimrod Mkono alisema wakandarasi hao hawana uwezo wa kujenga barabara hiyo bali wanastahili kuomgezewa nguvu ili kuweza kukamilisha barabara hiyo kwa wakati.

Mkono alisema mara kadhaa amekuwa akitoa ushauri kwa Serikali juu ya mwenendo wa ujenzi wa barabara hiyo lakini imekuwa kimya na kuna uwezekano mkubwa wa barabara hiyo kuchukua muda mrefu hadi kukamilika.

Post a Comment