BEN AKIWA NA MRISHO NGASA UWANJA WA TAIFA
KUONDOKA AIR PORT
NDANI YA NDEGE KUELEKEA BOTSWANA KAMBI YA TAIFA STARS
MFANIKIO HUANZIA KUANDIKWA NA VYOMBO VYA HABARI KWA MAZURI
KIPA wa timu ya
Taifa ya Tanzania(Taifa Stars) aliyeitwa kwenye kikosi cha timu hiyo kutoka
timu ya mkoa wa Mara kufutia jopo la makocha kusaka vipaji vya kuboresha Taifa
Stars, Benedictor Tinoko amesema amesajili Kagera Sugar ili kusaka namba kwenye
timu hiyo.
Akizungumza kutoka nchini Botswana ambapo timu hiyo imeweka kambi kwaajili ya maandalizi ya mchezo dhidi ya Msumbiji,Tinoko alisema amekwenda Kagera ili kucheza ligi kuu na kulinda kipaji chake ili aendelee kubaki Taifa Stars.
Alisema amesajili Kagera Sugar kwa mkataba wa miaka 2 kufuatia ushauri alioupata kutoka kwa makocha kutafuta timu ya ligi kuu ili aweze kucheza na kuonekana ambapo itampa nafasi zaidi ya kuendelea kuitumikia timu hiyo kwa kipindi kirefu.
Tinoko alisema akiwa
katika timu yake aliyosajili atajituma akiwa mazoezini na kwenye mechi ili
kuweza kutafuta nafasi ya kikosi cha kwanza ambayo ndio nafasi anayoikusudia
ili kuweza kuimalisha Zaidi kiwango chake.
Alisema kwa sasa
anajituma zaidi mazoezini akiwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa chini ya kocha
wa makipa Patrick Mwangata ambaye alimuona akiwa kwenye jopo la makocha ili
aingie kwenye maboresho ya Stars.
Kipa huyo ambaye
alianzia kuonekana kipaji chake kwenye timu mbalimbali za mtaani mjini Musoma
kabla ya kusajiliwa na timu ya Polisi Mara,alisema anamshukuru sana kocha
Mwangata ambaye kila siku amekuwa akimuhimiza kufanya juhudi mazoezini ili
aendelee kucheza mpira.
“Tangu tuko kambini
Mbeya kocha Mwangata amekuwa akinifatilia kwa karibu zaidi na kunitia moyo kila
siku na hata tulipofika hapa Botswana amekuwa akinisisitizia mazoezi naamini
siwezi kumuangusha bali ntaendeleza zaidi jitihada.
“Kuna makipa nimewakuta
hapa Taifa Stars na ni wazuri na mimi ntaongeza juhudi ili kuweza kupata nafasi
ya kucheza na nnashukuru kocha Mart Nooij anaendelea kuniona na
mechi ya juzi ya kirafiki dhidi ya Botswana nilikuwa kwenye benchi huku Dida
akiwa langoni,”alisema Tinoko.
Alisema jitihada zaidi
pia ataziongeza akiwa Kagera Sugar ili kuweza kujihakikisha nafasi kwenye
kikosi cha kwanza cha timu hiyo ambayo itakuwa fursa nyingine ya kuendelea
kuonekana.
Post a Comment
0 comments