0


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

JESHI LA POLISI TANZANIA

mso16A58

                                
TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI – 02.08.2014

1. AJARI YA GARI KUWAGONGA WAENDESHA PIKIPIKI   NA KUSABABISHA VIFO NA MAJERUHI:

Ndugu Waandishi wa habari; Mnamo tarehe 01.08.2014, majira ya saa 20:15hrs, Huko maeneo ya Kerasha,Kata ya Bweri, Tarafa ya Musoma,Manispaa ya Musoma, Mkoa wa Mara, Gari Namba T.861 ARZ aina ya NISSAN PICK-UP, lililokuwa likiendeshwa na NASSIBU S/O SHEDRACK, Miaka 31yrs, Mkazi wa Bweri, liliwagonga waendesha Pikipiki wawili na kusababisha vifo kwa watu watatu (3) ambao ni Dereva wa Pikipiki namba T.622 CKQ aitwaye RAMADHAN S/O WEREMA, Miaka 25, Mkazi wa Bweri na abiria wake wawili ambao ni 1. MAKEBO S/O ROKI, Miaka 24yrs, Mkazi wa Bweri, 2. MARIA W/O RAMA, Miaka 22yrs, Mkazi wa Bweri,Pia alimgonga mwendesha pikipiki aitwaye SAMWELI S/O MANUMBU, Miaka  42yrs, Mkazi wa  Songe, ambaye amevunjika Mkono wa kushoto na kupata majeraha katika miguu yote miwili na hali yake ni mbaya, na pikipiki aliyokuwa akiiendesha haijafahamika namba zake za usajiri kwani ilitoroshwa eneo la tukio.


Chanzo cha ajali ni Uzembe uliosababishwa na mwendo kasi wa dereva  wa gari ambaye alihama kutoka kushoto kwenda kulia mwabarabara, Dereva wa gari hilo naye amepata majeraha kwa kukatwakatwa na vioo vya gari na amelazwa hospitali ya Mkoa Mara akiwa chini ya ulinzi wa Polisi. Pia Dereva wa Pikipiki naye amelazwa katika Hospitali hiyo. Miili ya Marehemu imehifadhiwa katika hospitali ya Serikali ya  Mkoa  wa Mara.

WITO

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara; Anatoa wito kwa Madereva wote waendeshao magari pamoja na pikipiki kuwa waangalifu na kufuata sheria za usalama barabarani ilikuepusha ajari zisizo za lazima.

PHILIP ALEX KALANGI- ACP.
 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MARA-MUSOMA.


Post a Comment