0




EKWABI AKIPIGA KURA


EKWABI AKIPELEKWA MEZA KUU NA DIWANI WA ETARO BAADA YA KUSHINDA
EKWABI KULIA AKIPONGEZWA NA MWENYEKITI WA HALIMASHAURI YA MUSOMA


Ekwabi ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kutangazwa kushika kwa mara nyingine nafasi hiyo katika uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halimashauri ya Musoma baaday kupata kura 23 huku 1 ikiwa imeharibika.

Amesema ili kufanya halimashauri hiyo kufikia malengo kuhusiana na mipango yake,ni kuwa na umoja kiutendaji kwa pande zote zinazofanya kazi kwenye halimashauri ikiwemo kufanya jitihada za ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Makamu Mwenyekiti huyo wa halimashauri ya Musoma,ushindi wa kishindo waliompa madiwani wenzake kuendelea kushika nafasi hiyo ni ishara wana imani na utendaji wake wa kazi na kuomba kuendelea kuwa na ushirikiano madhubuti na kufanya kazi kama timu ili kufanikisha utekelezaji wa shughuli za halimashauri.

Amesema suala la msingi ambalo amewaomba madiwani kuwa na ushirikiano ni kuhakikisha ifikapo novemba 28 mwaka huu ujenzi wa maabara kwenye shule za Kata uweze kukamilika kutokana na walivyokubaliana kufuatia agizo la Rais Kikwete.

Ekwabi amesema kama hakutakuwa na ushirikiano baina ya madiwani wote na wananchi kwenye Kata hawataweza kufanikiwa kukamilisha maabara kama ilivyokusudiwa na wanafunzi kwenye halimashauri hiyo waweze kujifunza masomo ya kisayansi kupitia maabara hizo.

Aidha Ekwabi amesema wataendelea kuzingatia taarifa ya Mdhibiti wa Hesabu za Serikali(CAG) kwa kuhakikisha wanasimamia usimamizi wa usomaji wa mapato na matumizi kwenye Kata pamoja na ulipaji wa madeni ya wazabuni wanaofanya kazi kwenye halimashauri hiyo.


Post a Comment