0
 WANANCHI WAKIANGALIA KABURI LILILOFUKULIWA

 WANANCHI WAKIANGALIA KINACHOENDELEA
 KABURI LILILOFUKULIWA


   

WANANCHI wa Manispaa ya Musoma jana asubuhi walikubwa na hofu kubwa kufuatiliwa kutolewa kwa taarifa za kufukuliwa kwa kaburi moja la mtu aliyepata ajali iliyoua watu 37 eneo la Sabasaba wilayani Butiama. 


Mapema asubuhi wananchi hao walikusanyika katika eneo la makaburi ya Waislamu yaliyopo eneo la Musoma basi kushuhudia kaburi la marehemu aliyefahamika kwa jina la Juma Sai Mambina aliyekuwa mtumishi katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mara.


Babu wa Marehemu aliyefahamika kwa jina la Abuu Msonge akizungumzia tukio hilo eneo la makaburi,alisema walipata taarifa za kufufuliwa kwa kaburi hilo baada ya ndugu ambao hawakuwepo siku ya msiba  kwenda kuona kaburi hilo.


Amesema ndugu hao waliondoka eneo la msiba mapema alfajiri na walipofika eneo la makaburi walishangaa kuona kaburi likiwa limefukuliwa huku mbao ambazo hutumika kuzikia zikiwa pembeni na kuamua kutoa taarifa kwa ndugu wengine walioko nyumbani.


Msonge amesema baada ya kupata taarifa hizo walikwenda kutoa taarifa polisi ili kuweza kufatilia tukio hilo ambalo alidai kuwashangaza familia ya marehemu na kuanza kuibua vilio kutokana na tukio hilo.


“Jana ilikuwa tuanue matanga na kumaliza msiba,kuna ndugu ambao walikuwa mbali na hawakuwepo siku ya maziko,sasa leo waalipokwenda makaburini kuona kaburi ndio walipokuta limefukuliwa na kutoa taarifa nyumbani kuanza kulifatilia.


“Tulikwenda polisi na baadae Mahakamani kwaajili ya kupata kibari ili kwenda kuchunguza vizuri kama mwili ulikuwa ndani ya kaburi ama ulikuwa umeondolewa baada ya kufukuliwa kwa kaburi hilo la ndugu ndugu yetu Juma Sai.amesema Msonge.


Amesema baada ya kupata kibari walikwenda eneo la makaburi wakiwa na daktari pamoja askari na kulifukua kaburi hilo na kuukuta mwili ukiwemo huku ukiwa hauna pungufu lolote la kiungo na kuamua kuuzika tena kisha kutawanyika.


Babu huyo wa marehemu amesema wameshangazwa na tukio hilo na kudai waliofanya tukio hilo si watu wazuri kwa kuwa tayari walikuwa wameshamstili ndugu yao na kufanya hivyo kumewaumiza na hawajui lengo la wahusika hao.


Akizungumzia tukio hilo,Imamu wa Msikiti wa Taqwa Selemani Hamis aliyeshiriki kuuzika tena mwili huo alisema hakukuwa na pungufu lolote kwa maiti hiyo na kudaai huenda ni imani za kishirikiana zilizopelekea kufukuliwa kwa kaburi hilo.


Amesema si jambo jema lililofanywa na wahusika wa tukio hilo na kuitaka jamii kumuogopa Mwenyezi Mungu na kujiepusha na matukio ambayo si ya kawaida na yanayopelekea mtu kupata dhambi.


Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wameitaka jamii kuachana na mambo yasiyo ya kiingwana kwa kuwa kufufua kaburi kunawaumiza wafiwa na kudai kila mmoja awe mtoa taarifa pale anapoona tukio lisilo la kawaida ili wahusika waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Post a Comment