0



 SAMAKI WANAOFUGWA NA VIJANA WAKIONEKANA NDANI YA BWAWA
 SEHEMU YA VIJANA 280 WA KIKUNDI CHA IGWE WANAOLALAMIKIA MWENGE WA UHURU

KIKUNDI cha Vijana Wajasiliamli wafugaji wa samaki na kuku cha (Igwe group) kilichopo Kata ya Iringo Manispaa ya Musoma wamelalamikia waratibu wa shughuli za mbio za mwenge kuwasababishia hasara ya zaidi ya shilingi milioni 3 kwa kushindwa kuzindua miradi yao.

Wakizungumza katika eneo lao la bwawa la samaki,vijana hao walisema wamesikitishwa na viongozi wa Manispaa kushindwa kuzindua miradi yao wakati walikuwa wakiwahimiza kufanya taratibu ambazo zingefanya mwenge wa uhuru kufika kwao.

Walisema kabla ya mwenge kuanza kukimbizwa Manispaa ya Musoma septemba 9 walikuwa wakitembelewa mara kwa mara na viongozi na kulidhika na miradi yao ya ufugaji wa samaki na kuku zaidi ya 600 na kuwataka kujiandaa kupokea mwenge lakini cha kustajabisha haukuweza kufika na kuwapa hasara.

Mmoja wa vijana hao aliyejitambulisha kwa jina la Godfrey Kembo alisema wameshangazwa na viongozi wa Manispaa na kudai hawakuwatendea haki kuacha kuzindua miradi yao na matokeo yake kupelekea mwenge huo kufungua nyumba ya mtu binafsi ya kulala wageni na kuwaacha vijana 280 waliojiunga na kikundi kwa lengo la kuipatia kipato.

Alisema kutokana na kupangwa kwenye ratiba kuzinduliwa miradi yao walifanya maandalizi makubwa ikiwemo kuchapisha fulana,kuandaa chakula pamoja na kutengeneza miundombinu ya kufikiwa kwenye miradi yao na kushindwa kufika.

"Hili”jambo kama vijana limetuuma sana,tunaachwa vijana 280 tumejiandaa kisha inakwenda kufunguliwa nyumba ya kulala wageni na kwenda kuzindua mradi wa kuku 30,tutafikisha malalamiko yetu ngazi za juu gharama tulizoingia turudishiwe hawezi kutufanyia haya.

Mlezi wa kikundi hicho Juma Musuto alisema siasa imeingizwa kwenye shughuli za mwenge na uongozi wa Manispaa ya Musoma huenda umepokea maelekezo kutoka kwa wanasiasa na kufuta kwenda kuzindua miradi ya vijana ambao wameamua kujishughulisha.

Alisema vijana wamekichukulia kitendo hicho kwa masikitiko makubwa kwa kuwa waliamini mwenge kuzindua miradi yao ingewafanya kutambulika na kutoa hamasa kwa vijana wengine kubuni shughuli mbalimbali ambazo zinaweza kuwapatia kipato.

Post a Comment